Sunday, May 1, 2011

MEI MOSI MWAKA HUU WAFANYA KAZI WAMETAKIWA KUJIANDAA ILI BAADA YA KUSTAAFU WAISHI MAISHA MAREFU

 Mei Mosi mwaka huu kiwilaya imefanyika katika uwanja wa maji maji.Mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Songea Bwana Thomas Ole Sabaya.katika hotuba yake amewataka wafanya kazi waandae vyema maisha yao baada ya kustaafu kwao.Alisema wajiandae kiuhalali na sio kuiba maana watafungwa..
Mkuu huyo amewapongeza wote waliozawadiwa kwa kufanya kazi kwa bidii na wengine waige mifano yao,pia alisema wanaopata zawadi kweli wawe wanasifa sio zamu yao imefiaka wapewe.
 Mkuu wa Wilaya Bw.Sabaya anampa shilingi laki mbili na cheti mwali Eva Kazimoto wa shule ya sekondari Ruvuma.Mfanyakazi wa TANROAD ndiye aliyepata zawadi kubwa kuliko wote kwa kupata sh.700,0000.
 Maandamano ya magari ya taasisi mbalimbali zikielekea kupita mbele ya mgeni rasmi kuonyesha shughuli zao.
 Mfanyakazi akikabidhiwa sh.200,000 na cheti katika kilele cha Mei Mosi kilichofanyika kiwilaya katika uwanja wa majimaji  manispaa ya Songea leo.

No comments:

Post a Comment