Thursday, May 5, 2011

UHAKIKA UKOJE KUHUSU WASWAHILI NA HISTORIA YAO?


WASWAHILI lazima watakuwa na Historia yao ingawa si rahisi kuelezea bila kujua lugha yao ilianza lini na wapi karne gani.Wataalamu wa lugha ya Kiswahili wamechambua kuwa kwenye karne ya 18 au kabla yake maandishi ya Kiswahili ya aina Fulani yalianza kuonekana

Wachambuzi waliowengi wamadai Kiswahili kina asili ya Kibantu ambao labda walitokea Afrika Magharibi na jinsi walivyo zagaa Mashariki na Kusini mwa Afrika na namna walivyo jigawa katika makundi yao mbalimbali lakini cha ajabu historia haichambui vikundi vilivyo unda jamii hiyo bali marejeo mengi yanazungumzia jamii ya Wabantu kwa ujumla.

Marejeo yanazungumzia historia ya lugha na jamii ya waswahili kupitia enzi za nyuma katika kitabu cha Derek Nurse na Thomas Spear.walau kitabu hichi ndicho kinatoa mwanga kidogo kuhusu jamii ya Wabantu walioelekea mashariki na mahusiano yao na jamii zisizo za Kibantu.

Kila lugha ina historia yake na chimbuko lake,Watu wengi wanadhani Kiswahili ni lugha nyepesi,lakini ni nyepesi kwa kuongea bali si rahisi kwa wanafunzi,ugumu unaojitokeza ni upungufu wa vitabu vya rejea na ziada,na tatizo hilo ni kwa wanafunzi wa ngazi zote.

Kwa hiyo ukitaka kujua historia ya lugha na jamii ya waswahili ni lazima uwe na ushahidi wa kiakolojia na kihistoria kuanzia karne za nyuma hadi miaka 800 na ya 1500 B.K.Aidha marejeo yanabaini historia ya Kiswahili ilianza tangu karne ya 19 hadi 20.

Kiswahili hicho kikaanza kukuzwa katika nchi mbalimbali za Afrika Mashariki na kwa kiasi Fulani  Afrika ya Kati.Kama mwanzo wa Blogu hii nilileta Magofu ya miskiti na majengo ya Masultani ya Kilwa Kisiwani ambayo yalijengwa na Masultani wa Kiarabu waliofika kwa shuhguli za biashara na kueneza dini ya Kiislamu.

Tangu Milenia ya kwanza Pwani ya bahari ya Hindi ilijikita katika mazingira mapana ya biashara ambapo ngarawa zilisafiri kutoka Bara Arabu na Ghuba ya Uajemi zilizopeperushwa kila mwaka na pepo za kaskazi na kuleta vyombo vilivyo finyangwa,nguo na vyombo vya chuma.

Warabu hao walibadilishana na watumwa,pembe za ndovu,dhahabu,mbao,simbi,rangi na manukato,kisha walirejea kwao na zikipeperushwa na pepo za kusi.Ingawa bidha hizo zilikwisha fikishwa na Wareno na Wagiriki kabla ya karne ya tatu.

Ukisoma marejeo mengi,vitabu vya rejea na ziada utapata uhakika wa chimbuko la lugha ya Kiswahili katika Upwa wa Bahari ya Hindi  Afrika Mashariki ambapo wafanya biashara wa kiafrika na waarabu na wajemi walitokea kwenye bandari katika Ghuba ya Uajemi.Baadaye biashara ilihamia kusini – magharibi mwa Uarabu Yemen na Hadhramaut hatimaye Oman.

Baadaye tutaendelea  na biashara……….

No comments:

Post a Comment