Thursday, October 29, 2015

SHAMRASHAMRA KUMPONGEZA DKT JOHN POMBE MAGUFULI ZILITANZA KATIKA MJI WA MAKAO MAKUU YA CCM MJINI DODOMA ,MAGARI, PIKIPIKI ZIKIWA NA BENDERA ZA KIJANI,WAKIKSEMA HAPA NI KAZI TU.

Magari na pikipiki yakisimama kwa ghafla kupisha au kuruhusu vijana ,watu wazima ,akina mama na watoto wakiwa kwenye furaha za kupongeza ushidhi baada ya kutangazwa na Tume ya Uchaguzi .
Furaha zao zilifanywa kwa Amani na Utulivu,ambapo magari ya polisi katika mji huo yalionekana yakipita pita kuhakikisha amani inakuwepo kwa waliyo furahia matokeo na wale ambao upepo umewaendea kombo lakini wote ni watanzania na watabaki kuwa watanzania

TANZANIA IMEINGIA KATIKA HISTORIA YA KUTANGAZA MATOKEO YA URAIS KWA DKT JOHN POMBE MAGUFULI NA MGOMBEA MWENZA WAKE SAMIA HASSAN SULUHU KWA KURA 8,882,935. NA KUIWEKA TANZANIA KATIKA HISTORIA YA KUWA NA MAKAMU WA RAIS MWANAMKE,WATANZANIA WANATEGEMEA MABADILIKO KAMA WALIVYO ELEZA KWENYE SERA ZAO

 Rais Mteule  Dkt.John Pombe Magufuli leo ametangazwa rasmi  kuwa Rais  wa awamu ya Tano baada ya kushinda kwa kura 8,882,935 akifuatiwa na Mhe. Edward Lowassa kwa kura 6,072,848.

Kutokana na matokeo hayo Mgombea mwenza Mhe. Samia Hassan Suluhu anakuwa makamu wa Rais wa kwanza  mwanamke Tanzania,Hongera zao.Na kwamba kesho kuanzia saa 4. watatunukiwa Hati au Cheti cha hushindi.
Mhe.Samia Hassan Suluhu Mgombea mwenza wa Dkt Magufuli  kutokana na Sera zao wameibuka kuwa washindi kwa kura 8,882,935,kesho watatunukiwa hati ya ushindi katika ukumbi Diamond Jubelee Jijini Dar es Salam saa 4 asubuhi.Hongereni sana watanzania wanasubiri mabadiliko.

Monday, October 26, 2015

TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI YATANGAZA MATOKEO YA URAIS KUPITIA VYOMBO VYA HABARI ,NA KUTOA ANGALIZO

Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Jaji Mstaafu Damian Lubuva ameanza kutangaza matokeo ya Urais ambapo Kupitia CCM Dr. Joseph Pombe Magufuli anaonekana kuongoza akifuatiwa na wa CHADEMA Edward Lowassa.Jaji Lubuva amewaambia wandishi wa habari kuwa  kesho saa tatu asubuhi. ataendelea kutangza matokeo mengine yatakayo pokelewa kutoka  kwenye Majimbo ya uchaguzi nchini.

Aidha alisema kuwa mwenye mamlaka ya kutangaza matokeo ya Urai ni Tume ya Uchaguzi ya Taifa peke yake, mtu mwingine atakapo tangaza yatakuwa siyo matokeo rasmi.Na kwamba aliwaonyesha waandishi wa habari makaratasi yaliyo sainiwa na mawakala wa vyama vyao.na kutumwa Tume ili yatangazwe.

Saturday, October 24, 2015

KITUO CHA KUPIGIA KURA CHA OFISI ZA SHIRIKA LA NYUMBA LA TAIFA DODOMA SAA MOJA KAMILI WANANCHI WALIANZA KUPIGA KURA,KWA AMANI NA UTULIVU MKUBWA

  • Kuona jinsi wananchi walivyo hamasika wengi wamejitokeza kwa wingi kwenda kutimiza haki zao za msingi  cha chagua viongozi wanao wataka.
  • Mabasi yakutoka na kuingia kwenye stendi ya mabasi Mkoa wa Dodoma  hayapo wasafiri nao hawapo stendi imetulia kama vile watu hawapo.
  • Kwenye Zahanati ya Mkole nako hata wagonjwa nao hawapo pametulia.
  • Barabara na mitaa ya Mji wa Dodoma kumetulia .ukweli hali ni shwari.
  • Kituo hicho hali nishwari kabisa ,wanamama,wazee,na vijana wamejitokeza na wameelekezwa vya kutosha.

 Foleni ya wapiga kura katika kituo cha ofisi za Shirika la Nyumba na Taifa wakiwa katika kusubiri zamu zao  za kupiga kura zifike
  • Hii barabara ya kutoka Bungeni kuelekea mjini iko tupu
Foleni ya wapiga kura pamoja wa waandishi wa habari wako sambamba kufuatilia mwenendo mzima wa kupiga kura,akiwemo wa ITV na vymombo vingine li kuhabarisha Taifa na Dunia kwa ujumla kuonyesha jinsi Tanzania ilivyo kuwa na Ukomavu wa Vyama vingi na kuzingatia Democrasia ya kweli..


Hiki ni kituo cha Zahanati cha Makole kumekuwa na utulivu kama vile wagonjwa hawapo,lakini yote ni kwenda kupiga kura.

TUNAMSHUKURU MUNGU KWA KUANZA NA KUMALIZA KAMPENI KWA AMANI NA UTULIVU, HIVYO WATANZANIA KESHO WAKATIMIZE WAJIBU WAO ,KWA AMANI NA UTULIVU ULIOKUWEPO WAKATI WA KAMPENI

Viongozi wa wametumiza wajibu wao wa kunadi Sera zao wakati wa Kampeni kwa Amani ,Utulivu,Busara zilizotumika katika kuonyesha ukomavu wa Demokrasia wa Vyama vingi.

Hivyo ukomavu huo wananchi wautumie kumpata kiongozi ambaye atatimiza ndoto za watanzania.Ni imani yetu uchaguzi utaenda salama hapo kesho kwa kuwa uchaguzi unapita,baada ya hapo majukumu yetu yataendelea kama kawaida.

Tunaipenda Tanzania yenyebamani na n chi ya mfano wa kuigwa hivyo tuulinde mfano huo,Mungu ataepusha machafuko amabayo yanatokea kwenye nchi zisizo na Amani.Tujitokeze  kuanzia saamoja asubuhi tupige kura turudi nyumbani tusubiri matokeo.

Wednesday, October 21, 2015

WAKATI ZIMEBAKIA SIKU TATU WATANZANIA WATUMIE HAKI YAO YA KUCHAGUA VIONGOZI WANAO WATAKA MKURUGENZI WA HUDUMA ZA SHERIA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI BWANA EMANNUEL KAVISHE ASEMA MWENYE KUTANGAZA MATOKEO NI TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

Aidha Bw. Kavishe amesema Viongozi wa Vyama na wananchi wanatakiwa kupiga kura zao kwa amani na utulivu na kwamba ,baada ya kupiga kura watu warudi walikotoka na kusubili matokeo ambayo yatangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
Amesema Mtu atayepata kura nyingi atatangazwa kutoka kwenye chama chochote ambacho mgombea amepata kura nyingi.
kuhusu idadi kamili ya wapiga kura tarehe 25 mwezi huu ,amesema kuwa ni watu milioni 22..7 ambao wanatarajiwa katika upigaji kura siku hiyo,nakwamba kila mtu atapiga  kura kwenye kituo alichojiandikisha,na kama yuko nje ya kituo chake basi mtu huyo atakuwa amekosa haki yake ya kumchagua kiongozi anaye mtaka.
Pia kasema ili kuepusha vurugu zisizo na sababu wananchi wafuate maelekezo ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi,na kuheshimu Katiba.Na madai ya kubaki kwenye vituo baada ya kupiga kura, inamaana mawakala waliyowekwa na vyama vyao hawaviamini.maana waele ndiyo watao hakikisha mgombea wake amepata kura ngapi.

Saturday, October 17, 2015

WANAFUNZI 177 WA CHUO CHA UHASIBU CBM DODOMA KILICHOJULIKANA KAMA ASEK WAMEHITIMU KATIKA NGAZI YA STASHAHADA NA CHETI











Wahitimu hao wa 177 wakiwemo 102  wa Stashahada  na 75 wa Cheti katika fani za Procurement and Supply,Marketing,Banking and Financial and Accountancy  katika Chuo hicho jana 

Saturday, October 10, 2015

RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA JAKAYA KIKWETE AZINDUA KIWANDA CHA KUCHAKATA GESI MADIMBA MTWARA LEO

Nakwamba Rais amezindua viwanda vingine  vya Mtwara kikiwemo cha saruji,kiwanda kikubwa ambacho kitawanufaisha wananchi wa Kusini na majirani zao.

Tuesday, October 6, 2015

BLOG YA TUJIFUNZE KUSINI INATOA POLE KWA FAMILIA YA MWANASIASA MKONGWE MCHUNGAJI CHRISTOPHER MTIKILA ,PAMOJA NA WANASIASA KWA KUFUATIA KIFO CHA MWANA SIASA HUYO AMBAPO MCHANGO WAKE UILIKUWA BADO UNAHITAJIKA

Tukio la mwana siasa huyo limemshitua kila mmoja wetu , lakini hatuna uwezo zaidi wa kuamua lini na wapi na muda gani binadamu atatoweka duniani  na kwa mtindo gani,yote tumuachie Mungu kwani yeye ndiye mwenye kujua nani anamuhitaji kumchukua.
Hivyo Familia na wale wote wenye mapenzi mema kwa marehemu Mtikila kuwa na subira hasa kwa kipindi chote cha msiba huu,kwani Bwana alitoa na Bwana alichukua.Roho ya Marehemu Mungu ailaze mahali pema peponi Amina.

WAKATI ZIMEBAKI SIKU CHAHCE KUELEKEA UCHAGUZI MKUU WA MADIWANI,WAGUNGE NA URAIS,WATANZANIA WAMETAKIWA KUWA KUTUNZA SHAHADA ZAO ZAKUPIGIA KURA

Baadhi ya wananchi wenye kuipenda amani utulivu,pamoja na utulivu, upendo kwa atanzania wote kuacha kuwahadaa watu  wenye shahada zao za kupigia kura kuzifanya ziwe bidhaa kwa mafaniko yao katika kuchaguzi ujao.

 Aidha wanaomba wananchi kujitokeza kwa wingi kusikiliza Sera za wagombea mbalimbali wa vyama vyote ,ili wajue na wachambue mbivu na mbicha tarehe 25 mwezi huu.

Lakini sanasana cha muhimu ni kuaandaa mazingira ya Amani ,utulivu siku hiyo ya kupiga kura.Hasa kila mmoja amalizapo kufanya kitendo cha haki yake ya kumchagua Diwani,Mbunge na Rais tarehe 25, arudi nyumbani kwakwe kusubili matokeo.

Wale ambao wanatarajia kubakia vituoni kusubiri kuona aliyemchagua kashinda,waache kwani kufanya hivyo kutasababisha uvunjifu wa Amani.Nini maada ya mawakala wa vyama na Tume ya Uchaguzi,Kazi ya kutangaza matokeo ni Tume ya Uchaguzi wengine Turudi majumbani mwetu.

Inajulikana kuwa kura ni siri ya mpiga kura,sasa wewe mwingine kushabikia fulani lazima ashinde je wewe ulikuwa na wapigakura wote nchini ukaona wamemchagua huyo unaye sisitita kuwa kashinda ,jamani tuwaachie wenyewe watakao hesabu kura na kutoa matangazo.

Blogu hii imesikiliza maoni ya baadhi ya Wananchi wa Dodoma wakielezea mtazamo wao katika mwelekeo wa Uchaguzi mkuu tarehe 25 mwezi huu,na kwamba iwapo wananchi watafuata maelekezo ya Tume ya Uchaguzi na Vyombo vya Ulinzi na Usalama ,Uchaguzi siku hiyo utakuwa wa  Amani na Utulivu kwani Tanzania ni Kisiwa cha Amani.Hivyo tumuombe Mungu aifanye siku hiyo iwe ya Amani na Utulivu na Atuongoze katika kuwapata viongozi ambao ni chaguo lake.