Saturday, March 5, 2011

KUTANA NA VITUKO VYA KUTISHA NDANI YA ( NILITAFUNA WANANGU 10 )

Kitabu cha Irene Mwamfupe Ndauka ni kitabu kilichoandikwa kwa lengo la   kuelimisha jamii kuhusu uchawi na wachawi walivyo zagaa katika jamii aliyoiandikia kitabu hiki,lakini ni jamii nyingi za kiafrika zinaimani  imani za kishirikina  au  uchawi na kuchawia wengine.Ambao ni mbumbu katika sayansi ya kichawi.

Mtunzi wa hadithi katika kitabu hiki,mhusika mkuu amemjenga kama kweli ni mchawi,kwa kuanza kuua mkewe kwa lengo la kupata mavuno mengi ya miwa kwa kushawishiwa na jirani yake ambaye alikuwa mashuhuri kwa uchawi,baadaye akawa maarufu wa kula  nyama za watu,ndipo alipowatafuna watoto wake 10 mmoja hadi mwingine. Zaidi utayakuta ndani ya kitabu hiki ambacho kinasomwa ,Afrika Mashariki.

1 comment: