Tuesday, March 22, 2011

LIKIZO NAYO INAPENDEZA UKIWA NA FAMILIA NYUMBANI BAADA YA KUTOKA KWENYE IBADA

 Dodoma baada ya kutoka kwenye ibada ya Kristmas mwaka jana tulipiga picha ya pamoja na mke wangu kama ukumbusho wa kumaliza mwaka 2010 na kuukaribisha mwaka 2011.
 Tukiwa ndani Binti yangu Sarah alitaka kutupiga picha ya wima kama tunavyoonekana na Mrs.
 Mrs Sikapundwa na wanae na mie nikawa Camera man niliwapiga picha hiyo wakati wakivywa vinywaji baridi .
 Sarah alipiga pisha kaka yake Michael  Siakapundwa  mwalimu Diploma mwaka wa kwanza yeye hakupenda kukaa kwenye mkeka wakati wa kula chakula unajua kula kwenye mkeka kunahitaji mazoea.
Bwana Joseph Sikapundwa yeye ni Diploma Chuo cha Biashara Dodoma ( CBE ) anaweza kukaa kwenye mkeka wakayti wa kula kama anavyo onekana akishambulia kipande cha nyama 
 Miea na mke wangu tulikaa kwenye mkeka ,lakini nilipata shida sana kwa kuwa ni shida sana,ilinipasa kugeuka geuka.
Hata hivyo inapendeza kukaa chini kwenye mkeka kukaa kwenye meza wakati wa kula ni utamaduni tuliouiga kwa wageni,Mapokeo ya kibantu kitu meza hakikuwaepo,Hivyo siku mojamoja si mbaya kukaa kwenye mkeka.

2 comments:

  1. Safi sana hii kwanza ni kumbukumbu nzuri sana na pili ni kuendeleza utamaduni wetu. Kutama pa mpasa....

    ReplyDelete
  2. Safi sana Mzee Sikapundwa. Ninaandaa safari ya kuja huko Tanzania, na kitu kimoja ambacho nawazia mara kwa mara ni kuwa iwapo uko Ruvuma, labda tutaweza kuonana. Taarifa unazotuletea hapa kwenye blogu zinanikumbusha nyumbani vizuri.

    Sijui kama nilishakuambia kuwa mimi ni mwenyeji wa Litembo, lakini kwa hivyo hata haya maeneo ya Dada Yasinta ya Ruhuwiko na Mfaranyaki ni kwetu tu.

    Naona kwenye blogu unatupa picha mara kwa mara kuwa uko Dodoma, na papo hapo uko Songea. Sijui hasa unapatikana sehemu zote mbili kwa awamu au vipi.

    Shukrani kwa taarifa zote na picha.

    ReplyDelete