Sunday, March 20, 2011

MOROGORO KASORO BAHARI NA BAHARI INGEKUWEPO INGEKAUKA !! !

Hali ya hewa imeuathiri sana mkoa wa Morogoro,Morogoro ya leo si Morogoro ile ya mvua nyingi,milima ilikuwa ikitiririka maji,kwa ajili ya mvua nyingi,vyakula vilikuwa vya kumwaga ukianzia mahindi,mpunga,pamba na hata mtama vikiwemo viazi vitamu na mihogo.

Leo hii hakuna mvua ya uhakika katika mkoa huo,hazina ratiba ya kunyesha ya kuwafanya wakulima wajue ni lini wataanza kulima na kupanda.na ikinyesha siyo ya kuaminika inaweza ikakatika kabla ya mazao kukomaa.

No comments:

Post a Comment