Friday, March 25, 2011

MRADI WA YEBO YEBO HAUNA MASLAHI KWA WAMILIKI WA PIKIPIKI

Sintofahamu imewakumba vijana hawa walipo kutwa na gari la matangazo la Manispaa ya Songea kuwa wanatakiwa kulipia ushuru wa pikipiki za kukodisha ( yebo yebo ) katika manispaa shilingi 30,000 kila baada ya miezi sita.


Vijana hao walisema walizani kuwa kuendesha yebo yebo kungenusuru maisha yao kumbe imekuwa ni kuinusuru serikali kwa kukusanya ushuru kupitia yebo yebo hizo,walisema Mapato shilingi 95,000 kwa mwaka,BIMA shilingi 25,000 kwa mwaka na Halmashuri za Manispaa shilngi 30,000 kila miezi sita,bado polisi,matengnezo,mwenye pikipiki apate nini na dereva naye apate kitu gani ,je hiyo ndiyo ajira yenyewe?

No comments:

Post a Comment