Tuesday, February 15, 2011

KILWA NA BIASHARA YA WATUMWA NA HISTORIA YA KISWAHILI NA MAJENGO YA MATUMBAWE

 Sehemu ya jengo ambalo lilikuwa na ukumbi mkubwa wa kunadi bidhaa zikiwemo watumwa,pembe za ndovu,simbi,mbao na vyombo vya kufinyangwa kutoka bara la Arabu na Ghuba ya uajemi,kisha kuingiza kwenye ngarawa tayari kwa kusafirisha.
 Hicho ni kiberenge kilitumiwa na mmoja wa mwanaakolojia ambaye akikuwa akichimba ili aone masalia ya vyombo vilivyo kuwa zikitumika wakati huo na washirazi kisiwani hao wakati huo.aliyeshika kiberenge ni Bw.samweli mtembeza wattalii.
Hapo si kiwanja ila ni ukumbi amabo mnada ulikuwa ukifanyika,au sherehe zao watawala hao wa kiarabu walikuwa wakifanyia humo,kwa mbele kuna maji ni bahari ambapo kuna ngazi za kuteremshia bidhaa kuingiza kwenye ngarawa zao.fika ukajionee ni utalii nafuu zana wa kuona kisiwa cha kihistoria Tanzania.



Pwani ya kusini mwa Tanzania Mafia na kilwa ilikuwa ni miji ya biashara katika karne ya kumi na moja,pia biashara ilishamiri Mogadisho nchini Somalia.Ngarawa zilipeleka pembe za ndovu,dhahabu kutoka Msumbiji,watumwa na bidhaa kadhaa kutoka pande nyingine za pwani kwa ajili ya kuwauzia warabu wakati wa msimu wa biashara.

Aidha Kilwa kutokana na wanaisimu wanasema historia ya Kiswahili imeanzia miji ya pwani ya Afrika Mashariki,na Kilwa ni mmoja wapo.warabu waliingia kiujanja ujanja kufundisha dini ya kiislamu ambapo shehe wa kwanza alikuwa mshirazi Muhammad mtoto wa Ali bin Hasan.

Alikuwa mwanzilishi wa utawala wa Kilwa na kukutwa na Wareno,na ndiye aliyekuwa wa kwanza katika mlolongo wa Waarabu kutoka Bara la Arabu na Ghuba ya Uajemi.Ili kujua tamaduni na asili ya waswahili katika pwani hizo wanaakolojia wanachambua kwa makini ambapo wanaantropojia nao walifanya tafiti zao za kuchunguza mabaki katika miji na vijiji katika Pwani hiyo.

Mapema katika milenia ya kwanza kabla ya Kristo ngarawa zilikuwa zikisafiri kutoka Bara la Arabu na Ghuba ya Uajemi zikipeperushwa na pepo za kaskazi,kuleta vyombo vilivyofinyangwa,nguo na vyombo vya chuma vilivyo badilishwa na pembe za ndovu,watumwa,mbao,simbi na rangi na kurudi kwao na pepo za kusi.

Kwa wale wanaochukua shahada ya kwanza ya Kiswahili ningewashauri wafanye ziara kwenda maeneo yenye chimbuko la historia ya Kiswahili waone eneo warabu walopokuwa wakipakizia bidhaa zao kwenye majahazi wakiwemo binadamu maarufu watumwa kupelekwa bara Arabu na Ghuba ya Uajemi.

Ukifika utapata kuelewa mamwinyi na umarufu wao,kuliko kusoma tu kwenye vitabu,ustarabu na utamaduni wa kiafrka wa pwani hiyo na washirzi noa kuwepo kwa lugha ya Kiswahili,pia kuondoa dhana potofu ya kuwa asili ya Kiswahili ni kiarabu au kibantu kwa kuangalia lahaja zilizokuwa zikitumika pwani na wenzao wa bara.

Na kuyaona magofu yaliyojengwa kwa mawe matumbawe,yanye asili ya majengo ya kishirazi.yalikuwa majengo imara hadi leo ushahidi unaonekana,lakini kustawi kwa Kilwa Kisiwani kutakuwepo iwapo atapatikana mwekezaji wa kujenga hotel ya kitalii kwenye kisiwa hicho cha kihistoria,kilicho nunuliwa kwa kipande cha nguo kukizunguuka.

No comments:

Post a Comment