Monday, July 30, 2012

MWALIMU APEWA MKONG’OTO NA WANAFUNZI WAKE KWA KUFUNDISHA SIKU YA MGOMO WA WALIMU SONGEA



BADHI ya wanafunzi wa shule ya msingi Kambarage Halmashauri ya Manispaa ya Songea wamempatia mkong’oto mwalimu   aliyejulikana kwa jina la Kahimba kwa madai ya kuwa na kuherehere cha kufundisha wakati walimu wengine wapo kwenye mgomo ulifanyika nchi nzima,wakidai kuwa mwalimu huyo amewasaliti walimu wenzake na viongozi wa Chama cha Walimu Tanzania.
   Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Kambarage Bibi Adolophine Ndunguru katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea alithibitisha tulio hilo kuwa lilitokea majira ya asubuhi.
    Aidha Katibu wa Chama Cha Walimu Tanzania wa Mkoa wa Ruvuma Bwana Luya Ngonyani,alisema kuwa Mgomo wa Walimu ni halali umezingatia sheria ya ajira na mahusiano kazini ya mwaka 2004.
     Alisema kuwa hatua ya kwanza ya Chama Cha Walimu  (CWT ) imetekeleza kutangaza mgogoro wa siku 30 kwa kujaza fomu namba 1 kwa lengo la kudai  maslahi yao.
    Wakati Uongozi wa Manispaa ya Halmashauri ya Songea wakitaka kuitisha mkutano wa Waratibu Elimu Kata na Walimu wakuu wa shule wa Manispaa hiyo leo katika shule ya msingi Mfaranyaki uligonga mwamba baadaya wa Waratibu na walimu wakuu hao kuacha kwenda kwenye mkutano huo.
  Serikali isifanyie mzaha kuhusu tukio hilo,sio suala la kusema shauri lipo mahakamani ,walimu warudi shuleni kufundisha,Sekta ya Elimu ni Sekta nyeti si ya kuichezea chazea kama wengine wanavyo dhani,Mwalimu anaweza akapindisha Mtaala wa Elimu akafanya kinyume na Sera ya nchi kwa muda mfupi sana.Lakini watu hawaoni hayo." kilio cha walimu ni kurudishiwa Teaching allowance".

Saturday, July 21, 2012

WAFANYA BIASHARA WASISABISHE MWEZI RAMADHANI KUWA MWEZI WA MAJONZI NA MAJUTO BADALA YA FARAJA KWA WANAO FUNGA -SHEKHE JONGO

Shekhe Himidi Jongo akielezea umuhimu wa mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ambapo leo ni mfungo mosi.Aidha na kuwaomba wafanya biashara nchini kuacha kupandisha bidhaa bei.


Wafanya biashara wameshauriwa kuacha kupandisha vitu bei kwa sababu ya mfungo wa Ramadhani,Shekhe Hamidi Jongo wa Dar es Salaam alisema hayo kwenye kipindi maalumu cha TBC jana wakati akielezea umuhimu wa kufunga kwa waumini wa Dini ya Kiislam.
Alisema Mungu alihalalisha biashara kufanyika na aliharamisha riba katika biashara,hivyo kufanya bishara siyo dhambi  bali kupandisha vyakula wakati huu wa mwezi Mtukufu wa ramadhani ni dhambi kwani bei ya jana kabla ya mfungo kwa nazi,mhogo,mchele kwanini leo siku ya mfungo mosi ipande? ‘Wasifanye mwezi Ramadhani uwe ni mwezi wa Majonzi na majuto badala ya faraja kwa wanaofunga’ alisema Shekhe Jongo.
Aidha alisema kwa mfanya biashara wa Kiislamu awe mkweli kwa wateja wake wakifika kununua mchele au maharage asema kweli kuwa maharage yake yanaiva haraka au yanachelewa kuliko kusema maharage yake ni maji mara moja kumbe uongo.Mtu kama huyo asifunge maana atakuwa anapoteza muda wake bure.
Tuungane na Shekhe  Jongo kuwahasa wafanya biashara wa mhogo,maharage,nazi,tambi,tende wauze bidhaa hizo kwa bei ya halali,wasipandishe bidha hizo muhimu kwani kufanya hivyo ni kuwakomoa  wenzetu watakaojaliwa kufunga,kwani mwezi huu ni mwezi  Mtukufu kwa waumini wa Kiislamu.

Thursday, July 19, 2012

NI JAMBO LA KUFURAHISHA LA KUKUTANA NA BLOGGER MKUBWA NA KUCHATI NAE INAPENDEZA KWELI SI MWINGINE PROFESA MBELE - SONGEA LEO

 Baada ya mapumziko ya safari ya basi kutoka Dar es Salaam kuja hapa Songea Profesa Mbela mwenye shati la mistari pamoja na ndugu zake picha ya pamoja katika ukumbi wa Serengeti ,maarufu sana hapo Songea kwa kupata moja baridi na moto pia,
Hapa Prf.Mbele anajikumbusha kivywaji cha nchi yake almaarufu Kili- manjaro akiwa na Dada Sia  katika ukumbi wa Serengeti Manispaa ya Songea,Prf.Mbele pamoja na kuishi nchini Marekani kikazi,lakini hukumbuka kurudi nchini kwakwe na hasa mkoani kwake na wilayani kwake Mbinga.
Profesa Mbele anaamini kuwa usomi haupungui iwapo msomi akijichanganya na watu wa kawaida,na wala akiwa akiongea na vijana wa vijiweni,Hawampunguzii Uprofesa wake,maana kazi ya Mungu ni kubwa kwa kuwa siyoyote yanayo zungumzwa na watu wa kawaida ni vya upuuzi la,ila kuna mengine yana maana huenda hata alipokuwepo chuoni hakuwahi kusikia.
Mie na mpongeza sana Profesa huyo,kwa kuwa anatambua kuwa kila mmoja na mchango wake katika jamii kulingana na kiwango chake cha elimu au cha uelewa wake kasoma au hapana,endelea hivyo profesa Mbele kwa mtindo huo utachota mambo mengi yanayoizunguka dunia hii.

TUJIFUNZE KUSINI INATOA POLE KWA FAMILIA ZILIZO POTELEWA NA JAMAA ZAO KATIKA AJALI YA MELI HUKO ZANZIBAR

TUJIFUNZE Kusini pamoja na timu nzima ya TUJIFUNZE  ikopamoja katika majonzi ya wananchi wa Tanzania Visiwani pamoja na wananchi wa Visiwani ambao ndugu zao wamepoteza maisha katika ajali nyingine ya meli.Tunatoa pole kwa familia zilizofikwa na msiba huo.
Katika matukio kama haya wananchi tuwe na subira na uvumilivu kwa kuwa yote yanayotokea ni matakwa ya Muweza wetu.Na mara nyingi kunapotokea matatizo watu lazima watu watatupiana lawama.Cha msingi nikumuomba Mungu atuepushie jali za mara kwa mara,hasa zinazotokana na uzembe.

Tuesday, July 17, 2012

MATUKIO MJI WA SONGEA

Watu wawili wanao sadikiwa kuwa ni wazazi wa mtoto anyekaa katika maeneo ya Matogoro Manispaa ya Songea wametuhumiwa kumnyonga mtoto wao ambeya alianza kukaa,kwa mijbu wa kikosi cha jeshi la polisi mkoani hapa wazazi hao wanashikiliwa na polisi.
Tukio lingine Kijana ( 25 ) mwendesha pikipiki almaarufu yeboyebo mjini hapa amekutwa amekufa katika nyumba moja maeneo ya Bombambili Manispaa ya songea ,baada ya kutoonenaka kwa tajiri yake kwa siku tatu.inasadikiwa kuuawa na watu wasiyojulikana hadi sasa.
Tukio lingine ni la lori lililobeba mahindi kutumbukia katika daraja la Matarawe barabara ya kuelekea Mji mwema Manispaa ya Songea,Chanzo cha ajali hiyo bado kueleweka vyema hadi tunaenda mitamboni,hiyo ndiyo habari.

Saturday, July 14, 2012

WANANCHI KUTOA USHIRIKIANO KWA MAKARANI WA SENSA SIKU YA TAREHE 25 /8/2012 SIKU YA KUHESABIWA

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Mizengo Pinda alisema kuwa siku ya tarehe 25 mwezi wa nane mwaka huu makarani wa sensa watapita katika kaya za watu kuhesabu,kuelewa siku ya kuamkia tarehe 25 ni watu wangapi wamelala katika nyumba ile.
Aidha Mhe.Pinda alisema kuwa wananchi wajitokeze kutoa maoni yao kuhusu Katiba mpya siku Tume ya Katiba ikifika katika maeneo yao.
Mhe.Pinda alisema hayo siku akizindua mradi wa matrekta katika uwanja wa Zimani moto katika Manispaa ya Songea hivi karibuni,siku ya pili ya ziara yake ya siku mbili ya kikazi Mkoani Ruvuma.

Sunday, July 8, 2012

CHUO KIKUU CHA SAUT SONGEA KUANZISHA EVINING CLASS KUANZIA MWEZI WA 9 MWAKA HUU

               CHUO KIKUU CHA SAUT SONGEA KUONGEZA VITIVO

MSHAURI wa wanachuo ( Dean of Student ) Michael Sinienga alisema hayo hivi karibuni kwa waandhishi wa habari wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi wa Kanda ya Kusini walipotembelea chuo hicho kwa lengo la kupata taarifa za mafanikio na changamoto kadhaa tangu chuo hicho kianze kudahili wanachuo wake.
     Bwana Sinienga alitaja vitivo vitakavyo ongezeka kuwa ni pamoja na ‘Business Administration, Law, Medicine, Mass Communication  and Education’ ambayo ndiyo iliyoanza.
   Matarajio mengine ya chuo hicho ni kutoa kozi fupifupi za ujasiliamali, kozi za jioni ‘Evening classes’  kwa watumishi na watu wengine wenye kutaka kusomea shahada wakiwa kazini.
    Matarajio mengine ni kutoa huduma kwa shule za sekondari ambazo zitakuwa na uhaba walimu na zikipenda kupata huduma hiyo kutoka katika Chuo Kikuu hicho, Pia kuwaandaa vijana kujiamini na kujitambua na maadili kuwekewa kipaumbele.






Ziara ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda ya siku mbili mkoani Ruvuma





Serikali kuitoa asilimia 70 ya wakulima wa Tanzania wanaotumia jembe la mkono kwenda kwenye kilimo cha kisasa cha matrekta.

 Waziri Mkuu Mizengo Pinda watatu kutoka kulia akipungia wananchi mkono  wa kwaheri jana katika uwanja wa zimanimoto Katika Manispaa ya Songea baada ya kuzindua matrekta 53 yaliyokopeshwa kwa wakulima wa Mkoa wa Ruvuma.
 Baadhi ya Matrekta yaliyo kabidhiwa jana kwa wakulima wa wilaya za Songea Manispaa,Songea Vijijini,Namtumbo ,Mbinga na Tunduru ambako wengi waliyachukua mayterkta hayo
 Mhe.Pinda akizindua trekta lililo kopwa na Mkuu wa Koa wa Ruvuma Mhe,Said Thabit Mwambungu.
 Waziri Mkuu akisalimiana na viongozi na baadhi ya wananchi waliofika kumpokea uwanjani katika uwanja wa ndege Songea Juzi alipoa anza ziar yake ya siku mbili mkoani Ruvuma juzi.
Mhe.Mizengo Pinda.


Ili kuitoa asilimia 70 ya Wa- Tanzania wanaotumia jembe la mkono kwa kilimo,
Serikali imeweka mkakati wa kuhamasisha wakulima kutumia matrekta katika kilimo chao badala jembe la mkono.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mizengo Pinda alisema hayo jana katika uwanja wa Zimani moto katika Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma ,wakati wa kuzindua mradi wa matrekata 53 ambayo yamekopeshwa kwa wananchi na wakulima kwa lengo la kumtoa mkulima kutoka matumizi ya jembe la mkono.
Alisema serikali imeagiza zaidi ya  amatrekta 1,600 kutoka nchini India kwa mkopo ambayo yapelekwa mikoani kwa mpango wa kuyakopesha wananchi kwa bei nafuu ambayo yatalipwa ndani ya miaka mnne.
   Aidha alisema kuwa uwezo wa trekta ni kulima heka 25 hivyo mmliki wa trekta anaweza akakodisha kwa wakulima wengine nao wakaachana na jembe la mkono.
  Alisema Halmashauri na vyama vya Ushirika wachukue matrekta hayo ili wawezi kukopesha wananchi wanye kutaka kutumia trekta katika kilimo.
         Pamoja na mambo mengine Waziri Mkuu waliwahimiza wananchi kujitokeza kwa wingi wakati Tume ya Katiba inapofika katika mikoa yao ambapo Tume hiyo imeanza katika mikoa 8 isitosha alihimiza kwa wananchi usiku wa kumkia tarehe 25  mwezi wa 8 mwaka huu, kila mwananchi atahesabiwa ni siku ya Sensa Kitaifa ameomba wannanchi kutoa ushirikiano wa kutosha kwa makarani wa sensa wanapopita katika kaya zao siku hiyo.

Saturday, July 7, 2012

MIZENGO PINDA ATUA SONGEA KWA ZIARA YA KIKAZI YA SIKU MBILI KUANZIA JANA HADI LEO

Ashuka kenye ndege jana katika uwanja wa ndege wa Songea ,Nakisha akasalimiana  na viongozi na kuvishwa Skafu na mwanafunzi Mercy Ngatunga wa Sekondari ya Matarawe.Baadaye akaelekea Ikuli kusomewa taarifa ya maendeleo ya Mkoa na Taarifa ya Chama Tawala ( CCM )



WAZIRI MKUU MHE,MIZENGO PINDA AZINDUA NA KUGAWA MATREKTA 33 KATI YA 53 YANAYOKOPESHWA KWA WAKULIMA WA MKOA WA RUVUMA,KUONDOKANA NA JEMBE LA MKONO

 Waziri Mkuu wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Mizengo Pinda leo amezindua mradi wa matrekta 53 na kati ya hayo 33 yameshapata wanunuzi ambao wamekabidhiwa fungu na Mhe Waziri Mkuu katika viwanja vya Zimani Moto Songea leo.
Baada ya kukata utepe Waziri Mkuu alijaribu kuliwasha trekta lililokopwa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mhe.Said Thabit Mwambungu.
Aidha alisema matrekta hayo lazima yapelekwe shambani,si vinginevyo,na kwamba amewataka Halmashauri zote nchini kupunguza utitiri wa vikwazo vya mazo katika barabara.
Waziri Mkuu alikuwa akiwaonyesha watu namna trekta linavyo weza kuwa msaada na ukombozi mkubwa kwa mkulima.

Thursday, July 5, 2012

CHUO KIKUU SAUT TAWI LA SONGEA KUONGEZA KUWA NA VITIVO VITANO KUANZIA SEPTEMBA 2012

Profesa Donatus Albert Komba akiwa Ofisini kwake katika Chuo Kikuu cha SAUT Tawi la chuo Kikuu cha SAUT Mwanza Mjini Songea.kk






\[CHUO KIKUU TAWI LA SAUT CHA SONKUANZIA SEPTEMBER 2012
MKURUGENZI  wa chuo hicho Profesa Donatus Albert Komba alisema hayo ofisini kwake leo kwa waandishi wa habari waliyotembelea chuoni hapo katika Manispaa ya Songea, kuona na kupata maelezo ya mafanikio ya chuo hicho ambacho ni tawi la chuo kikuu cha SAUT cha Jijini Mwanza.
Profesa Komba alisema kuwa chuo kinatarajia kuwa na vitivo sita kuanzia mwezi September mwaka huu,alivitaja vitivo hivyo kuwa ni pamoja na ‘Education, Law, Business Administration,Sociology, Mass Communication, and Medicine’.
Alisema kuanzia mwezi Septemba 2012 chuo kitapokea wanafunzi wanafunzi wengi ikilinganishwa na sasa wachache ambao ni 176 kati yao wavulana108 na wasichana78.na walimu 13 na wafanyakazi ambao si walimu 17.
Kuhusu ada inayolipwa katika chuo hicho ni Tshs.2,600,000 kwa wanafunzi wa Kitivo cha Medicine ambapo Bodi ya mikopo huwakopesha kiwango chote hicho kutokana na umuhimu wao.
Aidha kwa vitivo vingine ada ni Tshs.950,000 kwa mwaka ambayo hulipwa kwa awamu mbili.ambapo Bodi ya mikopo huwakopesha Tshs.475,000/= kiasi kinacho salia hulipa wenyewe.
Alisema kuwa wanfunzi 50 wa kitivo cha Medicine kitaanzia Songea wakati miundombinu ya chuo kikuu cha tiba ikikamilishwa Peramiho,ikikamilika watakwenda kuendelea na masomo yao kwa mika mitano huko Peramiho.
Hilo ni jengo la Utawala la chuo kikuu cha SAUT Songea

.