Tuesday, December 31, 2013

HANDING OVER THE CERTIFICATE OF HAND OVER TO JUMA T, NYUMAYO





Handing over the certificate of hand over to Mr Juma T. Nyumayo as a new Editor of Southern Zone.Ruvuma,Lindi and Mtwara.

Friday, December 27, 2013

KILA CHENYE MWANZO HAKIKOSI KUWA NA MWISHO.HII NI SIKU AMBAYO ILIKUWA YA MWISHO WA UTUMISHI WANGU WA UMMA KANDA YA KUSINI







WATOTO WA SHULE YA AWALI CHARITY UWANJA WA SABASABA SONGEA WAMALIZA ELIMU YA AWALI

Mgeni Rasmi Bwana Bakule bakule maarufu kwa kuwa na timu yake ya miguu Matarawe Songea aliahidi kutoa mchango wake wa shilingi laki mbili.
Aidha alisema kuwa elimu ya Awali ni muhimu sana kwa kuinua taaluma hasa shule za English Medium,na kwamba alisema wakaze uzi wa kuendeleza watoto hao hadi darasa la saba
 Baadhi ya mwanafunzi wa Awali akimkabidhi shairi Mgeni Rasmi siku hiyo ya Awali
 Wanafunzi hao wakisoma shairi bila kubabaika utadhani darasa la saba kumbe ni watoto wa Awali

Baadhi ya wazazi wa watoto waliyo maliza elimu ya Awali siku hiyo

Thursday, December 26, 2013

Kifo cha mtoto Jems Steven wa mwaka mmoja na miezi miwili cha kinyama chashitua wakazi wa mtaa wa nanenane katika Manispaa ya Morogoro leo

Mtoto Jems Steven wa Mtaa wa Nanenane katika Manispaa ya Morogoro akutwa amekufa wakati mwili wake umefunikwa na takataka za mto Morogoro akiwa amekatwa sehemu zake za siri ,kidole na kuchomwa na kitu chenye ncha kali katika paji la uso.
Kwa mujibu wa mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa Bw. Isack Ilomo ,anaema mtoto huyo alipotea jana jioni wakati mama yake mzazi alipo mwacha akinywa uji wakati yeye alienda kuchota maji nje ya nyumba yao ya kupanga,
Alisema mama huyo baada ya kuona mwanae hayupo aliwauliza wapanagaji wenzake kama wamemwona mtoto wake ,nao walikataa kuwa hawaja mwona wala kumwona mtu aliyeingia chumbani mwake kwani ni muda mfupi tu alipo mwacha mtoto huyo.
Alipeleka taarifa kwenye uongozi wa Serikali ya mtaa,Uongozi ulikwenda kwenye kituo kidogo cha polisi kuomba kibali cha hufanya upekuzi ili kubaini kama kuna mtu alimficha kwa malengo yaliyojitokeza. Polisi walikataa kutoa kibali wakidai mpaka baada ya masaa 24 ndipo kibali kitolewe.
Baada ya masaa hayo wananchi wameukuta mwili wa mtoto huyo pembeni ya kijito cha Morogoro akiwa amekufa.Kutokana na kifo hicho cha kusikitisha kimefanya wananchi wa mtaa huo kukilaumu kituo cha polisi kwa kukataa kutoa kibali kama wananchi wa mtaa huo walivyo omba,kwani walivyokuta  maiti hiyo ilikuwa bado ina joto,ni dalili kuwa kitendo hicho kilifanywa baada ya masaa hayo 24.Ambapo ni leo.
Ifike mahali sheria nyingne za Jeshi la Polisi zilegezwe ,maana raia hawezi kufanya upekuzi wa nyumba hadi nyumba bila ya search warrant.kama wangeruhusu wangeokoa maisha ya mtoto huyo.kwa vyovyote vitendo vilifanywa na majirani palepale hasa wapangaji wenzake.
Mwili wa Mtoto huyo umesafirishwa kwenda kuzikwa kijijini kwa wazazi wake mbele ya Biahawana Mkoani Dodoma Jioni hii leo kwa mazishi.Mungu ailaze roho ya Marehemu Jems Steven mahali peme peponi Amein.

Monday, September 9, 2013

SERIKALI YAAGIZA MIKOPO YA ELIMU YA JUU IRUIDISHWE ILI WENGINE

 Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe.Dkt Shukuru Kawambwa akiongea na wahitimu wa Stashahada na Shahada ya Kompyuta Sayansi katika chuo cha St,Joseph Songea leo wanachuo 96 wamehitimu mafunzo hayo.




 Picha ya pamoja ya wahitimu wa Shahada ya kwanza katika Kompyuta Sayansi
 Picha ya pamoja ya wahitimu wa Stashahada
Picha ya pamoja ya wahitimu wa Stashahada

 Wahitimu wakila kiapo kabla hawajatunukiwa Stashahada na Shahada zao.
Mawaziri wakimsikiliza mtoa maelezo kwenye chumba cha Kompyuta sayansi



SERIKALI imewataka wanafunzi wa elimu ya juu ambao wanakopeshwa fedha na Bodi ya mikopo nchini kuirejesha mikopo hiyo,mara tu  wanapo malize elimu yao na kufanikiwa kupata ajira, kwa kulipa mikopo hiyo kuitafanya serikali kuweze kuwakopesha wanachuo wengine.
Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Kawambwa kwenye mahafali ya nne yaliyofanyika St, Joseph  College of Information Technology Ruhuwiko nje kidogo ya Mji wa Songea leo.
Alisema serikali inahitaji kutoa elimu ya juu kwa wanachuo wote wenye sifa na vigezo vya kujiunga na vyuo vikuu nchini,na itajitahidi kutoa mikopo kwa kadiri ya uwezo wake ingawa idadi ya wanafunzi wanaodahiliwa ni wengi,kwa hiyo waliyo kopeshwa wakirejesha mikopo hiyo wanachuo wenye kuhitaji mikopo hiyo watapata.
Aidha ameto rai kwa waajiri kuonyeshe ushirikiano wao na serikali  katika kukusanya fedha hizo kwa wahitimu ambao wamewaajiri, kurejesha mikopo hiyo kwenye bodi ya mikopo.na wasipo fanya hivyo hatua kadhaa zitachukuliwa zidi yao.
Alisema serikali imetengenga shilingi trioni 1.45 kwa wanafunzi wa elimu ya juu,Wizara kupitia elimu ya juu na bodi ya mikopo imeamua kuongeza kiwango cha mkopo kwa mwanafunzi wa elimu ya hiyo.
Katika mahafali hayo wanachuo 96 wamehitimu mafunzo yao na kutunukiwa Stashahada kwa wanachuo 39  katika Fani ya Uhandisi wa Sayansi ya Kompyuta na 58 shahada ya kwanza katika Uhandisi wa Sayansi ya Kompyuta.

Sunday, August 25, 2013

TAFRIJA YA BWANA NA BIBI DICKSON D. NACHENGA ILIENDELEA KWA KEKI KUKATA NA KULISHANA NA SHUGHULI NYINGINE






















BWANA DICKSON D.NACHENGA AAMUA KUACHANA NA UKAPERA BAADA YA KUMPATA WITNESS JUMA TAFRIJA ILIKUWA HIVYOOOOOOOOOO

 Bwana Dickson D.Nachenga na Mkewe Bibi Witness Juma wakiwa wakitambulisha wazazi wa Mke
 Utambulisho uliendelea
Maharusi wakisalimia wahisani waliosababisha tafrija ifane
 Familia upande wa bwana harusi
 Wahisani wakienda kuwatakia heri
 kwa  upole Bibi Witness akimwegemea mmewe

 Ni ishara ya busu hili lakini mie sikulionna


 Maharusi kwenye chakula



 Wazazi kwenye chakula
Baadhi ya wahisani wakishudia tafrija hiyo ya kufana