Thursday, December 25, 2014

IBADA ZA CHRISTMASS MJINI DODOMA ZIMEFANA SANA NA ZIMETAWALIWA NA MAHUBILI YALIYOSHEHENI AMANI,UPANDO NA MSHIKAMANO PAMOJA NA KUWAKUMBUSHA WAUMINI HAO KUJITOKEZA KWA WINGI WAKATI WA UCHAGUZI WA WABUNGE NA URAIS,BAADA YA IBADA NI KUWA PAMOJA NA FAMILIA NYUMANI KWA VYAKULA NA VINYWAJI NA WATOTO

Wajukuu wa kwanza kushoto ni  Karen Michael Sikapundwa  na wapili ni Ester Emanuel Sikapundwa wakisheherekea Christmass kwa soda na chakula .Hivyo ndivyo ilivyo kama picha zote zinavyo someka.
Bibi Chris Baby Boy Emanuel akiwa na Mjukuu wake
Karen & Ester
Bwana Emanuel Sikapundwa Na Mtarajiwa wake na watoto wao Ester & Chris Baby Boy na Karen Michael Sikapundwa
Mr& Mrs Neson Mwakyusa na Familia yake siku ya Christmass tarehe 25/12/204 Dodoma


Mr.Mwakyusa Watoto na Wajukuu siku ya Christmass Mjini Dodoma






















Wednesday, December 24, 2014

BLOG YA TUJIFUNZE KUSINI INAWATAKIWA WAUMINI WA KIKRISTO KOTE DUNIANI MKESHA WA CHRISTMASS NA HERI YA MWAKA MPYA WA 2015.PIA KUSHEREHEKEA KWA AMANI NA UTULIVU.NI MATUMAINI YANGU VITENDO VYA UVUNJIFU WA AMANI HAUTA KUWEPO.

Nina mshukuru Mungu kwa kunilinda pamoja na Familia yangu ya Sikapundwa kuwa na afya njema.Bloggers wote heri ya Christmass na Mwaka Mpya wa 2015.
Tusheherekee kwa amani na Utulivu wanaokwenda kwenye Ibada ya Usiku wasiondoke wote nyumbani maana wengie hutumia mwanya wa sikukuu hizi kufanya uhalifu.

Friday, December 19, 2014

438,960 KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2015,KATIKA SHULE ZA SEKONDARI ZA SERIKALI KWA AWAMU MBILI AMBAPO AWAMU YA KWANZA ASILIMIA 97.23 NA 12,432 WAKOSA NAFASI

Naibu Waziri wa Elimu Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI Kassim Majaliwa alisema hayo mbele ya vyombo vya Habari hivi karibuni Jijini Dar es Saam ,na kwamba wanafunzi hao ni wale waliyopata daraja la A hadi C.
Alisema wanafunzi waliyokosa nafani katika mikoa ya Dodoma wanafunzi 9,824,Dar es Salaam wanafunzi ,1,414,Morogoro 752,Mtwara 281 na Katavi 161 kwa upungufu wa vyumba vya madarasa.
Aidha alisema kuwa wanafunzi 10,331 wamepata alama za daraja A ambapo wanafunzi 98,789 wamepata alama za daraja B,342,272 wamepata daraja C,321,939 daraja D wakati wanafunzi 18,787 daraja E.
Hatimaye Naibu Waziri huyo ameaasa wanafunzi wote kutumia fursa hiyo kwa kutumia muda wao katika kusoma,pia katoa pongezi kwa wadau wote wa elimu walio fanikisha ufanisi katika matokeo hayo kwakuonyesha alama za juu kwa wavulana ilikuwa 243 na wasichana alama  240 kati ya alama 250 kwa mwaka huu tofauti na mwaka 2013 ilikuwa alama 244.

Sunday, December 7, 2014

MHE. MBOWE ANGURUMA VIWANJA VYA BARAFU MKABALA NA UWANJA WA JAMHURI DODOMA MANISPAA UKITANGULIWA NA MAANDAMANO YA AMANI KUANZIA VIWANJA VYA DODOMA SEKONDARI WAKIGAWA VIPEPERUSHI VYENYE UJUMBE MZITO " OPERESHENI ONDOA CCM DODOMA " OCD

 Hivyo ndivyo vibwagizo vya UKAWA Kwa njia ya vipeperushi vyenye Ujumbe huo,katika harakati za kupata ushindi ndani ya Vyama vya Upinzani ,Hiyo ndiyo michezo ya Siasa.
 Ni maandamano ya Amani yaliyo anzia viwanja vya Shule ya Sekondari Dodoma kuelekea Viwanja vya Barafu Mkabala na Uwanja wa Jamhuri katika Manispaa ya Dodoma leo.
Matukio hayo ni kufuatia Maandalizi ya Uchaguzi wa Viongozi wa Serikali za Mtaa unaotarajia kufanyika nchi nzima hivi karibuni.
 Gari la Matangazo na pikipiki
 Hao ndiyo Makamanda wakiwa na Mtundiko kuashiria kwamba CCM inaondolewa Madarakani na Upinzani inashika madaraka hasa kwa ujumbe wa vipeperushi  vilivyo sambazwa Mjini hapa,Lakini ni  dalili za kujiamini.
 Hayo ni maandamano ya pikipiki ya wanachama wakiwa na bendera za CHADEMA ,CUF na nyingine kutokana na Vyama vilivyounda UKAWA
 Hapa Makamanda wakiwa wana pasha pasha mvuto kwa wananchi kusogea kwenye tukio hilo la Kihistoria kama mtangazaji alivyo kuwa akitangaza kuwa ni tukio la Kihistoria la kuitoa CCM madarakani kwa kuwapa likizo isiyo na malipo, Siasa Inapendeza masikioni.Haya kazi kwao tunawatakia mafankio mema katika safari yao ya Kuiondoa CCM kama vile imelala fo fofo.
Ni baadhi ya Viongozi.Zaidi utapata kutoka viwanja vya Barafu kwenye Magazeti na Luninga.

WAJUMBE WA BODI YA "MUTUAL GENERATION OF TANZANIA ( MGT) " IMEWAKILISHA MIRADI YAO MBELE YA WALEZI WAO MIRADI ILIYOFANYIKA NA INAYOTARAJIWA KUFANYWA KATIKA UKUMBI WA 56 KATIKA MANISPAA YA DODOMA NA MWENYEKITI WA MGT BWANA FERDINAND EMILY

 Wajumbe wa BODI ya Mutual Generation of Tanzania ( MGT ) Wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kumaliza kikao chao kifupi cha kuwakilisha Mirada iliyofanyiwa kazi na inayotarajia kufanyiwa kazi.












Mwanyekiti wa MGT Bw. Ferdinand Emily akilezea malengo ya Mutual Generation of Tanzania ( MGT ) mbele ya walezi  na wajumbe wa Shirika hilo lililoundwa na wanafunzi wa vyuo vikuu vinane Tanzania ambavyo ni Dodoma UDOM, Dar es Salaam UDSM,Chuo cha Elimu ya Biashara CBE, Makumira, Usimamizi wa Fedha  ( IFM), Mipango ( IRDP ) ,SUA na Chuo kikuu cha Jordan
 Walezi wa MGT aliyesimama na kusifu na kuelekeza juhudi za MGT ni Mkurugenzi wa AFNET Sarah D. Mwaga,wa kulia kwake ni Prof. Kalafunja Osaki wa UDOM ,wakatikati ni mwenyekiti wa MGT Bw. Ferdinand Emily , wa kushoto wake ni Bw. Christian Sikapundwa Stationery mkabala na Bohari ya Mkoa wa Dodoma na wanyuma Bi.Zaituni Said Ngwanga Kaimu Mwenyekiti MGT.
 Aliyesimama ni miongoni mwa walezi wa MGT Bi Mirium Zablon wa Sahara Media Group akiwapa moyo wa kujitoa katika kuanzisha Shirika hilo lisilo la Kiserikali la Wasomi waliohitu masomo yao na wale ambao bado wapo masomoni,akito wito kuwa wale ambao hawajajiunga na MGT wajiunge ili wajenge dhana Kujiajiri baada ya masomo yao. Ambapo mpaka sasa wajumbe waliyondani ya MGT ni zaidi ya 1000 idadi ambayo ni ndogo kulingana na idaidi ya wanafunzi wote walioko katika vyuo hivyo vinane nchini.
Wajumbe wa MGT wakisiliza kwa makini ushauri na mapendekezo yaliyokuwa yakitolewa na walezi hao moja baada ya mwingine.

MGT imeandaa mradi wa shule ya Sekondari ambayo itawapa fursa kubwa ya kufanya sekodari hiyo iweza kujiendesha yenyewe .Aidha imeanzisha mradi wa ufugaji wa kuku ambao uko tayari kinacho hitajika hapo ninamna ya kupata mtaji. Pia wameandaa miradi mingine itakayo kidhi  mahitaji ya watanzani ikiwemo ufugaji wa nyuki.


Tuesday, November 4, 2014


RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE,AHIMIZA VIJANA KUJITOKEZA KUGOMBEA NAFASI MBALIMBALI ZA UONGOZI KWA SERIKALI ZA MITAA,KWA KUWA NI SAFARI YA UWEKEZAJI WA UONGOZI KWA VIJANA

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na wazee wa Mji wa Dodoma leo,baada ya kukabidhiwa Risala iliyo somwa na Katibu wa Baraza  la wazee Shekhe Abdalah Makubeli.kisha ilikabdhiwa na Mwenyekiti wa Baraza hilo Balozi Job Lusinde.
Mwenyekiti wa Baraza la wazee wa mji wa Dodoma Balozi Job Lusinde amkabidhi Rais Jakaya Kikwete risala ya wazee hao iliyo mpongeza kwa ufanikishaji wa shughuli alizozifanya za maendeleo katika Awamu ya nne ya uongozi wake.


Katibu wa Baraza  la  wazee mkoa wa Dodoma Abdalah Makubeli alisoma Risala  kwa niaba yao wazee hao.
I .Walishukuru kwa kukubaliwa kuongea nao ,Aidha Risala hiyo ilielezea ( Suala la kukua kwa uchumi, kuinua uchumi Mkoani Dodoma na  taifa  kwa ujulma ,Kutuwezesha katika kilimo cha zabibu, viwanda ili kutoa ajira kwa vijana wetu.

Katika usindikaji wa mafuta ya kula na vya  nyama.  Pia walilisemea Suala la Makao makuu lipewe Msukumo  pamoja na kuiomba kuangalia Bodi ya SDA ili kusaidie ustawisishiji wa mji wa Dodoma.

Walisemea kuhusu ,muundo wa kusimamia Ardhi na makazi, na kuweka wazi ratiba ya utekelezaji na ustawisishaji wa Makao Makuu. Hivi sasa mkoa  unakuwa kwa kwasi. Mf kujengwa vyuo vikuu vikubwa katika Afrika mashariki na hivyo wameomba kuipa  Hadhi kuwa mji wa Dodoma na kwa wa  kimataifa.napia liwe  jiji.

Wamesema kwa kuwa miundombinu yake ni bora inayo kidhi mahitaji ya kuwa Jiji kama Majiji mengine nchini.

Sisi wazee tumeona upo umuhimu wa kushukuru maisha ya mama na watoto tunaomba kukamilisha ujenzi wa jingo katika Hospitali ya mkoa lililo jengwa kwa miaka 9 bila kukamilika,kwa ajili ya mama na watoto kwenye hospitali hiyo ya Rufaa ya mkoa.na kwamba wazee hao wameomba kupatiwa huduma ya afya jirani.

Sambamba na   hayo hawakusaha Kumpongeza kwa  kuanzisha mchakato wa Katiba pamoja na vikwazo vingi.vilivyojitokeza na hatimaye Katiba iliyopendekezwa akakabidhiwa,hivyo wameomba akamilishe kabla ya kuachia ngazi na kuongezea wananchi   wajitokeze kwa wingi katika kuipigia kura ya ndiyo katiba iliyopendekezwa.

 Na hatimaye Balozi Lusinde Mweyekiti wa Baraza la wazee Dodoma  alimkaribisha Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete.kuongea na wazee wa Dodoma.

Na Rais anasema.wazee mkutano huu wameitisha wenyewe.,ningekutana nanyi lakini nilikuwa na mambo mengi.Katika kujibia Risala ya wazee hao alisema atayashughulikia na kuyafuatilia yote waliyo yaomba. Yajiwemo kwa uwekezaji  wa Hoteli,Viwanda, ili kuongeza ajira kwa vijana wao. ,Ujenzi wa jingo la hospitali ya Mkoa wa Dodoma na huduma za afya kwa wazee.na uwezekano wa kuwa Dodoma kuwa Jiji.

.Ndipo alipozungumzia mambo manne muhimu

 Alisema kuwa mahusiano yetu na China ni mazuri ambapo alipokelewa vizuri sana kwa hafla maalumu ya kutimiza miaka 50 ya mahusiano ya Serikali ya Tanzania na.Serikali ya China  ambayo iliwakilishwa na  na Makamu wa Rais na hatimaya kukutana na Rais.alisema nusu karne ya mahusiano yetu yamekuwa na mafanikioa makuwa sana.

Rais aliwahimiza wananchi kujiandaa katika  uchaguzi wa Serikali za Mitaa.TAMISEMI wamesha anza    maandalizi ya kuandaa Ratiba ambazo zimeshatolewa.kwa majina ya mitaa,na Vitongiji.

Amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kwenda kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura, aidha wakati wa kupigia kura Katiba iliyopendekezwa wananchi wajitokeze kwa wingi kwenda kupiga ya ndiyo . kwa ajili ya vizazi vyetu vijavyo.
Aidha amewataka wenye sifa kujitokeza kugombea uongozi kwenye Serikali za Mitaa watu wazima,Vijana na wanawake wasibaki nyuma kujitokeze kugombea afasi hizo.

Alisema vijana wajitokeze kugombea uongozi kwa kuwa jimo wapo ya uwekezaji katika uongzi “ ni lazima tuanze safari ya uwekezaji katika uongozi” alisema Rais.

Jingine alizungumzia Katiba iliyopendekezwa,” ni Katiba iliyo kidhi  viwango vyote,ingekuwa kwenye mpira tungesema imekamilika katika Idara zote,Katiba ni nzuri” alisema.

.






Monday, November 3, 2014

VIKAO VYA BUNGE VITAANZA HAPA MJINI DODMA HAPO KESHO

Kwa mujibu wa Katibu wa Bunge kwa waandishi wa habari Mjini hapa kuwa kesho Bunge litaanza vikao vyake ambapo waheshimiwa wabunge wameanza kuingia mjini Dodoma kwa ajili ya vikao hivyo vya Bunge.

WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE INCHINI LEO WAMEANZA MITIHANI YA KUMALIZA ELIMU YA SEKONDARI

Tujifunze kusini Blog inawatakia wanafunzi wa kidato cha nne mitihani mema,Aidha inawaombea Mungu awaepushe na vishawishi vya udanganyifu wa mitihani katika kipindi chote cha mitihani yao.

Saturday, October 18, 2014

"MTOTO HATUMWI DUKANI LEO, NA AKITUMWA ATASAHAU CHENJI" HAYO NI YA LEO BADO MASAA MACHACHE TU WAPENZI,WASHABIKI WA YANGA NA SIMBA WATASHUHUDIA MTANANGE BAINA YA WATANI HAO WA JADI UWANJA WA TAIFA KUPITIA TBC 1

Wapenzi hao wameonekana wakijigamba kwa aina tofauti tofauti ya kila mmoja kumshinda mwenzake,lakini wanasema msema kweli ni dakika 90. Na kiingilio ni poa kabisa kisingizio kisiwepo tena kwa mashabiki wa soka.

BREAKING NEWS, MTIA AINA YA MSUFI ULIYOANGUKA KWA UPEPO MIAKA MITATU ILIYO PITA WILAYAI UYUI MKOA WA TABORA UMEINUKA NA KUSIMAMA KAMA ZAMANI, WANANCHI WAUVAMIA KUBANDUA MAGOME YA MTI HUO KWA IMANI ZA KISHIRIKINA

 Kwa mujibu wa TBC 1 kwamba mti huo aina ya msufi ulianguka kwa upepo mika mitatu iliyopita ikiwa na baadhi ya mabome ya mti huo pamoja na mti kwenye matawi ulishambuliwa na mchwa.Lakini majuzi tu mti huo ulionekana ukinyanyuka polepole kama vile kuna watu wana unyanyua hadi ukasimama kama awali.

Shuhuda mmoja Bi Saada yeye alisema aliuona na kusikia aina fulani ya sauti wakati mti huo ukisimama,watu waliojumuika kushangaa maajabu hayo wilayani Uyui Mkoa wa Tabora hivi karibuni  walionekana wakibandua magome ya mti huo,pamoja na udongo uliolalia mti wenyewe. ( Waswahili husema ukishangaa ya Musa utayaona ya Firauni. ).


DODOMA YETU LEO






UZINDUZI WA CHANJO YA SURUA, MINYOO,NGIRI MAJI KITAIFA MKOANI DODOMA KUFANYIKA NYERERE SQUARE ( VIWANJA VYA MWALIMU NYERER ) KWA MAANDAMANO YALIYO ANZIA BOHARI MKOA

 Brass Bend ya Jishi la Wananchi wa Tanzania
 Brass Bend hiyo ndiyo iliyoongoza maandamano kuelekea Nyerere Square yakianzia Bohari Mkoa Dodoma jirani na stendi kuu ya mabasi.
 Baadhi ya wanafunzi wauguzi kutoka Mirembe Mkoani Dodoma
 Wauguzi wanafunzi
 Wanafunzi wa shule za msingi za Manispaa ya Dodoma
Brass Bendi ya wanafunzi wa shule za msingi katika Manispaa ya Dodoma
 Maandamano
 Wanafunzi wa shule za English Medium katika Manispaa ya Dodoma
 Baadhi ya wanafunzi wa shule za sekondari katika Manispaa ya Dodoma

Pamoja na hao pia ni wanafunzi wa sekondari,Cha ajabu walengwa ambao ni Wanawake na Wanaume ambao ndiyo wanakuswa na  Uzinduzi wa Chanjo hiyo Kitaifa kwenye maandamano hawapo.

Aidha imekuwa ni mazoea katika baadhi ya mikoa kujiunga kwenye maandamano yanayo walenga wananchi moja kwa moja.Sana sana ni wanafunzi na wahusika wanaokuwa na wanafunzi hao.

Swali kama wanafunzi ,wanavyuo hawapo hayo maandamano hayatakuwepo?,kwanini maadamano ambayo hayawaletei tija wa faida wananchi wanakuwa wengi.Uzuri wake maandamano ya aina huyo wanafunzi hawa husishwi.

Hivyo kwakuwa hatuna utamaduni wa kuwa kwenye maadamano kama hayo au ni vipi ,bali tumekuwa wepesi wakwenda kwenye sehemu ya tukio kusubiri maandamano yaingie ambayo ni ya wanafunzi wa shule za msingi,sekondari na vyuo.na kwamba mgeni Rasmi anayapokea maandamano hayo ya wanafunzi, na katika hutuba yake hagusii kuhushu wananchi kujihusisha na maandamano yenye manufafaa kwa jamii zao,kuliko kuwaachia wanafunzi peke yao.

Tuesday, October 14, 2014

JAMII YA BLOG YA TJIFUNZE KUSINI NA FAMILIA YA SIKAPUNDWA WANAUNGANA NA WANANCHI WA TABORA KWENYE SHEREHE YA KUZIMA MWENGE NA KUTIMIZA MIAKA 15 YA KIFO CHA BABA WA TAIFA MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE



Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere leo ni mika 15 tangu atagulie mbele za haki.Mwaka ambao Tanzania inaanza safari ya Kihistoria ya kutuga Katiba itakayo wapeleka watanzania kwa miaka 50 ijayo.
Aidha siku yaleo ni siku Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Mrisho Kikwete alipozimwa Mwenge baada ya kukamilisha mbio zake nchi nzima na kuzindua na kuwekea mawe ya msigi miradi kadhaa ya miradi kadhaa ya maendeleo.

Wednesday, October 8, 2014

RAIS JAKAYA KIKWETE ,DR. SHEN WAKABIDHIWA KATIBA INAYOPENDEKEZWA MJINI DODOMA MBELE YA MABALOZI MBALIMBALI WALIYO HUDHURIA SHEREHE HIZO

 Rais Jakaya Kikwete na Dr. Shein waonyesha Katiba inayopendekezwa baada ya kukaidhiwa na mwenyekiti wa Bunge maalumu la Katiba Mhe.Samweli Sitta katika sherehe ya kukabidhi Katiba katika uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma leo.
 Mwenyekiti wa Bunge maalumu la Katiba Mhe. Samweli Sitta ,kielezea mafanikio na changamoto zilizojitokeza wakati wa kujadili Rasimu ya Katiba hiyo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr.Jakaya Kikwete asema Katiba inayopendekezwa ni halali, nzuri na hana wasiwasi nayo.Alisema Katiba ni nzuri haina mfano wake,amesema Katiba iliyomgusa kila mmoja na hali yake.
Aidha alisema Katiba imependekeza mambo megi ya Muugano ya kuwa na Serikali mbili,Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itakuwa na mamlaka kamili ya kupata mikopo bila Serikali ya Muungano,Kujiunga na Taasisi za kimataifa na kuondoa migogoro ya Muungano.
Kawataka watanzania kuisoma vizuri Katiba hiyo na kuielewa na hatimaye kupiga kura ya ndio.
 Naye mawkilishi wa Kundi la walemavu Mhe. Mpanju amempongeza Rais Kikwete kwa uadilifu wake aliyouonyesha kipindi cha majadiliano ya Ibara mbali mabli kuliko sababisha sintofahamu kadhaa ,kwa baadhi ya wajumbe na kususia lakini aliona kazi itaendelea kwa mujibu wa sheria iliyopangwa.
Alisema katiba hiyo imayajali makundi yote yakiwemo ,walemavu,wakulima,wanawake,wafugaji ,wavuvi,wasanii, na wachimbaji wadogo wadogo.
Baadhi ya wananchi waliyokuwa wakiingia ndani ya uwanja wa Jamhuri kushuhudia  tukio hilo la Kihistoria

Saturday, September 27, 2014

VIPEPERUSHI VYA KUTISHIA WANANCHI NA WAJUMBE WA BUNGE MAALUMU VYA SAMBAZWA NA WATU WASIYO JULIKANA KATIKA MANISPAA YA DODOMA JANA VYEYE VICHWA VYA HABARI OFAUTI

Hapa ni eneo la Bohari Mkoa wa Dodoma ambapo kuna ulinzi mkali wa polisi kwa ajili ya kuzuia  maandamano kuelekea Viwanja wa Bunge kusababisha vurugu.

Baadhi ya vipeperushi hivyo kilicho patikana na Blog hii inasema." ONYO Dodoma si mahali pa kufuga wezi wa fedha za Umma.Utakayeingia Bungeni kuanzia kesho,yatakayo kupata utajuta" mwisho wa kunukuu. Hivyo  vilisambazwa jana.
Lakini ilikuwa ni kelele za mlango,wajumbe wa Bunge Maalumu waliendelea na shughuli zao kama kawaida na hakuna chochote kilicho tokea kifuatia vipeperushi hivyo.

Thursday, September 18, 2014

VIJANA WANASEMA MAANDAMANO HAYANA NAFASI KWAO KWA KUWA HAYATAWASAIDIA KWENYE KUTATUA MATATIZO YAO YA AJIRA

 Vijana wa hawa wanawashangaa UKAWA ambao walitaka kufanya maandamano kuelekea Bungeni hapa Dodoma.Vijana hawa wamejiajiri katika uuzaji wa matunda
Huyu Kijana na mwenyekiti wa Bodaboda katika manispaa ya Dodoma akielekea kijiweni kwao.Ambapo hawa wamejiajiri kwenye bodaboda.

 Matunda nayo ni muhimu ambayo yamekuwa ni ajira kwa vijana

Kijana huyu amejiajiri na hapa yupo ofisini kwake.