Saturday, October 18, 2014

BREAKING NEWS, MTIA AINA YA MSUFI ULIYOANGUKA KWA UPEPO MIAKA MITATU ILIYO PITA WILAYAI UYUI MKOA WA TABORA UMEINUKA NA KUSIMAMA KAMA ZAMANI, WANANCHI WAUVAMIA KUBANDUA MAGOME YA MTI HUO KWA IMANI ZA KISHIRIKINA

 Kwa mujibu wa TBC 1 kwamba mti huo aina ya msufi ulianguka kwa upepo mika mitatu iliyopita ikiwa na baadhi ya mabome ya mti huo pamoja na mti kwenye matawi ulishambuliwa na mchwa.Lakini majuzi tu mti huo ulionekana ukinyanyuka polepole kama vile kuna watu wana unyanyua hadi ukasimama kama awali.

Shuhuda mmoja Bi Saada yeye alisema aliuona na kusikia aina fulani ya sauti wakati mti huo ukisimama,watu waliojumuika kushangaa maajabu hayo wilayani Uyui Mkoa wa Tabora hivi karibuni  walionekana wakibandua magome ya mti huo,pamoja na udongo uliolalia mti wenyewe. ( Waswahili husema ukishangaa ya Musa utayaona ya Firauni. ).


No comments:

Post a Comment