Sunday, July 12, 2015

NITUMENI NITAWATUMIKIA,KWA NGUVU ZOTE,MOYO WOTE - DKT JOHN POMBE MAGUFULI

 Hotuba yake Magufuli baada ya kutangazwa
Wajumbe wa Mkutano huo


Dkt John Pombe Magufuli alisema hayo baada ya kutangazwa kuwa mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano  wa Tanzania.
Aidha alisema kuwa yuko tayari kunadi Ilani ya CCM, na kwamba wenzake 38 atakuwa nao pamoja katika kuinadi Ilani ya Chama hadi ushindi unapatikana. Kwani Chama kwanza,CCM kwanza na Tanzania kwanza,ni lazima kuwa kitu kimoja.
Baadaye kamtangaza Samia Suluhu Hassan kuwa mgombea mwenza,na kuweka Hitoria katika Ramani ya Dunia kuwa na Mwanamke  wa kwanza Tanzania kuwa mgombea mwenza mwanamke.
Hatimaye saa 10 jioni leo Dkt Magufuli atanadiwa katika uwanja wa Jamhuri Mjini Dodoma na Juma nne Dar es Salaam.

HATIMAYE DKT JOHN POMBE MAGUFULI ASHINDA KWA KURA 2,104 NA KUPONGEZWA NA DKT ASHA ROSE MIGIRO BAADA YA KISHINDO CHA USHINDI

Dkt John Pombe Magufuli  ndiye aliyepata nafasi kupitia Tiketi Chama chake kuwa mgombea Urais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania,kwa kupigiwa kura na wajumbe wa Mkutano mkuu wa CCM,kwa kupata kura 2,104,ambapo Balozi Amina Said Ally kwa kura 253 na Dkt Asha Rose Migiro kwa kura59.

Wote wapo tayari kambi zao kuwa bega kwa bega na Dkt John Pombe Magufuli kuhakikisha ushindi unapatikana kwa Dkt Magufuli wa kupeperusha Bendera ya CCM.Na mwenye kiti wa Chama hicho.