Saturday, September 19, 2015

WASHABIKI ACHENI TABIA ZA KUCHANA MABANGO YA WAGOMBEA NAFASI MBALIMBALI ZA UONGOZI KATIKA UCHAGUZI MKUU UJAO HIVI PUNDE MWAKA HUU

Blogu hii imekuta baadhi ya wananchi katika Manispaa ya Dodoma wakilaani vikali kitendo cha kuchaniwa bango la mgombea ubunge wa Jimbo la Dodoma mjini kupitia CCM hivi karibuni nyakati za usiku,na kwamba kitendo hicho hakikuwapendezesha watu wenye hekima na busara zao mjini hapa.
.
Wanasema vitendo hivyo havina tija wala faida kwao na pengine watu hao hawajui thamani za vitu.Wanajiuliza walikuwa na tatizo gani na bango mpaka kulichana, wamesema mambo ya uchaguzi ni ya mpito tu baada ya hapo hali itaendelea kama kawaida,sasa aliyefanya kitendo hicho anapokutana na mgombea huyo atakuwa na amani moyoni mwake.

Aidha walisema vitendo hivyo havifai kama ndiyo ushabiki wa aina hiyo basi haufai kwakuwa ni vitendo vinavyo ashiria uvunjifu wa amani na upendo. katika Jamii ya Kitanzania na Duniani kote

Kufuatia kauli ya viongozi wa ngazi ya juu wa ulinzi na usalama wa mkoa huu,kwamba la kumtaka kila mwananchi akisha piga kura siku hiyo arudi nyumbani kwake kusubili matokeo,Kauli hiyo kwa watu kama hao inaweza kugonga mwamba kwa kutaka kubakia vituoni kusubiri matokeo.

Alisema watu  watakao kiuka agizo hilo asishangae kuona vyombo vya usalama vitapo mshughulikia kikamilifu maana atakuwa ameyataka mwenyewe kwa sababu ya ushabiki,hawajui ushabiki una weza kusababisha machafuko ya kupigwa na hata vifo vya kujitakia.Hivyo wenye tabia kama hizo waziache maana zita waletea wananchi kukosa amani kwa ajili ya watu wachache wasiye taka kusikia.

Tuesday, September 1, 2015

RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA JAKAYA MRISHO KIKWETE AAGWA NA VYOMBO VYA ULINZI NA USALMA KATIKA UKUMBI WA DIAMOND JUBILEE JIJINI DAR ES SALAM


Ameagwa na vyombo vya ulinzi na Usalama Diamond Jubilee Jijini Dar es Salaam na kupewa zawadi ya Trector na majembe yake ambapo Mama Salma Kikwete  amepewa zawadi ya ng’ombe wa maziwa.
Katika hotuba yake na vyombo hivo amewashukuru sana,kasha akasema anaondoka ikiwa watu bado wanampenda.
Aidha alisema anauhakika kuwa vyombo vya Ulinzi na usalama vipo katika hali nzuri, vikiwa na zana za kivita  imara, kujenga  Air Force imengwa,nyumba 10000 zinajengwa  ikiwa nyumba 6,000 ni Askari wa kawaida ambapo nyumba 4,000 ni za Mofisa wa ngazi za juu ,wakati na chini.
Jesha la polisi wanaletewa magari ambapo mipango imesha fanyika Nchini India,magari hayo muda wowote yatawafikia Jeshi la Polisi.
Magereza wao bado kupanga mapendekezo yao,amewaambia wafanye haraka kabla hajaondoka aidhinishe ili atakaye mpokea amkabidhi.
Alisema alichofarijika nalo ni la Umoja wa vyombo vya Ulinzi na Usalama,Kuboresha maslahi ya watumishi wa Umma na Vyombo vya Usalama.
Usipo wekeza kwenye vyombo vya ulinzi na Usalama ,Unaweka rehani maisha ya wananchi,pamoja na ughali wake lazima kuwekeza kwenye vyombo vya Ulinzi na usalama kwa usalama wa ulinzi wan chi na watu wake.
Kama vyomba ulinzi na usalama ni dhaifu mali zote zitahujumiwa bila kujua.Meli mbili zimeanza kulinda kwenye bahari yenye kina kirefu.
Uimara wa uchumi wan chi lazima ulindwe na Jeshi lake na uchumi ule lazima ulindwe kwa upanga.msipowekeza kwenye ulinzi na usalama ,mabenki yote yataibiwa kila siku.
Alisema Dunia sasa inabadilika kwa Sayansi na Teknolojia,lazima na majeshi yetu yafikie huko,Mf moi kumenunuliwa mashine yenye thamani ya Dollar milioni 2, ili kuokoq mqisha ya wananchi ,ukiogopa aghali huwezi kuokoa maisha ya wanachi.
Aidha alisema mwaka huu kuna uchaguzi,vyombo vya ulinzi na usalama hasa Polisi,kuhakikisha upigwaji kura unakuwa wa usalama ,hategemei kuwa kutakuwa na matukio ya kulishinda jeshi la Polisi.
Anastaafu atarudi  kuwa raia maarufu, Hawezi kwenda kuomba atoe ushauri kwa Rais,maana Rais washauri wake. Akitaka ushauri ataenda kuomba ushauri wa kulima mananasi yake,alisema Duniani hapa amefanya kazi kubwa ya Urais.siwezi kuomba kazi,kwa manufaa ya nchi yake kama ataombwa ushauri nitakuwa tayari.
Amesema kuwa walikuwa ndiyo nguzo yake,mhimili wake,kama walivyo msaidia na kumshauri atakaye atayeshika madaraka.kama walivyomshauri na nchi iko shwari.