Monday, August 31, 2015


MGOMBEA URAIS KUPITIA CHAMA CHA ACT WAZALENDO BIBI ANNA MGHWIRA AHAIDI KUUNDA SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA AKIJUMUISHA VYAMA VYOTE NA MAKUNDI YA KIJAMII

 Mgombea Urais kwa tiketi ya Chama cha ACT Bibi Anna Mghwira  akitaja misingi ya Utu,Uadilifu na Uzalendo katika Chama chake,Jana katika Viwanja vya Mbagala Jijini Dar es Salaam  katika Uzinduzi wa Kampeni ambapo amesema ataunda serikali ya Umoja wa Kitaifa kwa kujumuisha Vyama vyote mradi wawe na Utu,uadilifu na Uzalendo.
Baadhi ya wananchama waliyo hudhuria katika mkutano huo wa uzinduzi wa Kampeni ya ACT katika Viwanja vya Mbagala Jijini Dar es Salaam jana

 
Mgombea Urais huyo alisema hayo wakati  akizungumza na wanachama wa chama hicho katika viwanja vya Mbagala Jijini Dar es Salaam leo.
Amesema kuwa iwapo atapa ridhaa ya kuwa Rais wa awamu ya Tano ataunda serikali ya umoja wa Kitaifa kutoka vyama vyote,wananchi na Sekta mbalimbali kwa msingi wa kujali Utu,Uadilifu na Uzalendo.
Ametaja vipaumbele vyake ni pamoja na Hifadhi ya Jamii,Tatizo la ajira kutokana na  uwekezaji katika kilimo,Kuimarisha Makao makuu ya Dodoma kuwa ya Serikali,siyo ya Chama.kwani Dodoma ni katikati ya nchi makao makuu ya chama yatatafutiwa sehemu nyingine.
Vingine ni pamoja na hifadhi ya jamii,viwanda vya mazao ya kilimo,uvuvi utalii na michezo,nakwamba maliasili zote zitakuwa za wananchi na sio za Katiba,pamoja na kuboresha Elimu kwani watoto wanamaliza Elimu ya Msingi hawawezi kusoma na wale waliomaliza Elimu ya sekondari hawawezi kusoma barua ambapo wanaomaliza vyuo vikuu hawawezi kujieleza katika ofisi wanazofanyia kazi.
Aidha amesema kuwa watoto wengi wenye vipaji  wako mitaani wanaitwa watoto wa mitaani, serikali yake watoto wote hao watapata elimu.
Alisema iwapo atapata ridhaa hiyo ya kuwa Rais Mwenye kiti wa Chama hicho Bwana   Zitto Kabwe atakuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Awali Kampeni Meneja wa Chama hicho,ni mkakamavu na shujaa anayesema mambo asiyo na uhakika nayo yanayo sababisa kuingilia Utu wa mtu,lakini katika Sera zao wanajali utu,Uadilifi na Uzalindo katika Ilani yao ya Uchaguzi, kutokana na kauli ile ya kudhalilisha utu wa mtu vinaendana na wanayoyanadi.Kitu kile hakipendezeshi watu.Anatakiwa kunadi Ilani na Sera ya Chama chake siyo kukosoa kwani wana uhakika gani kama wakipata ridhaa kutawala watateleza ahadi zote kwa wananchi. Walizo zisema..
Kwa Stahili ile Chama cha Mapinduzi CCM kitaendelea kutawala  kwa muda mrefu kwa kuwa vyama vya Upinzani badala ya kusaidiana katika kunadi Sera zao wanazarauliana wao kwa wao.
Lakini kwanini  wanashambuliana wao kwa wao wakati wanadai kuleta mabadiliko katika Siasa,wakidai CCM imekaa madarakani kwa muda mrefu bila mabadiliko.Nimeamini kuwa vita vya panzi furaha ya kunguru.
Ukweli ndoto ya Ukawa kwenda Ikulu kwa Stahili ya msemaji wa ACT Wazalendo  ambaye ni Kampeni meneja haipo,kwani itawachanganya hata wananchi ambao nao walikuwa na ndoto ya madiliko wakachagua kuendelea na CCM hiyohiyo.kwa inaonyesha kuwa vyama hivyo kila kiongozi anataka madaraka ya juu.
Ila Mgombea wao anajua kutetea Sera na Ilani ya Chama chake,amepanga vipaumbele vyake kwa ufasaha na hakuwa na haja ya kuwalaumu wenzake au viongozi wailiyo shika madaraka ya juu.






Friday, August 21, 2015

WAGOMBEA UBUNGE KWA TIKETI YA CCM NA CHADEMA MJINI DODOMA UMEPAMBA MOTO KAMERA YATU IMEPATA MSAFARA WA MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA DODOMA MJINI WA CHADEMA AKIENDA KUCHUKUA FOMU KWENYE OFISI ZAO

 Baadhi ya gari lenye wapambe waliokuwa wakimsindikiza mgombea Ubonge kwa tiketi ya CHADEMA Jimbo la Dodoma Mjini kwenda kuchukua fomu kwenye Ofisi yao.
Sasa kimeeleweka maagizo ya kuacha ushabiki wa mbwembwe katika kusindikiza wagombea umeeleweka,


PAMOJA NA USHABIKI KWA WAKEREKETWA ,CHA MSINGI HAPA NI KUWA NA SHAHADA YA KUPIGIA KURA

Ushabiki wa kusindikiza viongozi kwenda kuchukua Fomu na kurudisha Fomu,uwe wa amani na nidhamu bila kujali Itikadi za vyama vyao.

Kinachao takiwa kutolewe elimu kwa mashabiki hao, siku ya kupiga kura wasijae kwenye vituo vya kupigia kura na kudai wanamtaka nani,kelele kibao waache. wawaachie mawakala wafanye kazi yao.

Maana mkono wa Dola ni mrefu kupita kawaida,watapigwa bila faida yoyote kwani huyo watakaye mtaka kuwa Diwani, Mbunge au Rais  akichaguliwa au hakuchaguliwa watapa faida gani au hasara gani.

Ushabiki usio na tija hauta saidia,Wananchi wengi wanaomba kwa Mungu kuwepo na Upigaji kura wa Amani,Ili Tanzania Ibakie kuwa kisiwa cha Amani.

Wengine wanasema hata viongozi nao waache lugha za kashfa wakati wa Kampeni zao,Matusi,lugha za kejeli,Ubabe na umwamba kwenye Kampeni hazisidii wananchi,Wananchi wanacho hitaji ni maisha nafuu, kumtoa mtanzania mwenye kipato cha chini na kumpeleka kwenye kipato walau hata cha kati na sio wimbo uliyozoeleka kila Awamu.

Tunawatakia Amani,Utulivu,Upendo na kuhasehimiana wakati wa Kampeni zao kwa kila Chama kilichoingia kwenye  kinyang'anyilo cha Udiwani,Ubonge na Urais