Monday, March 14, 2011

LEO SIKU YA PAI DUNIANI

Wanafunzi wametakiwa kuhamsishwa kupenda hisabati,hisbati ni somo linalofundishwa kutokana na mazingira,somo hilo si gumu bali huwa wanafunzi wanakatishwa tamaa na wenzao,ama wao wenyewe wakijenga hofu kuwa ni gumu.

Wasichana wanaweza sana somo hilo,lakini imebainika kuwa baadhi ya wavulana wasiolipnda somo hilo wanawakatisha tamaa.

Somo hilo ni rahisi halihitaji kukariri,bali ni kuelewa kanuni na njia za kufanya hesabu,mwanzo walimu wa hisabati akiingia darasani Introduction yake ni kuuliza wanafunzi maswali mafupimafupi ya orodha au table 1 hadi 12hivyo ilimlazimu mwanafunzi kuziimba orodha kwa kichwa.

Na pai walimu wa somo hilo wanafundisha kwa nyimbo,na zipo kwenye CD mwenyekiti wa somo la hisabati ameandaa CD hizo ,hivyo walimu wa somo hilo wazinunue ili ziwasaidie katika kufundisha pai.

No comments:

Post a Comment