Tuesday, March 1, 2011

MAONI WA WANANCHI WALIO ONGEA NA BLOGU HII MJINI MOROGORO,RUVUMA NA MBEYA KWA WAKATI TOFAUTI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jaakaya Mrisho Kikwete akiongea na  Wa - tanzania Mjini Dodoma.Pia alihutubia Bunge Jipya,na kama kawaida yake kuonge na wananchi kupita vyombo vya habari, wananchi wame toa maoni mengi sana kuhusu mstakabali wa  kujenga Taifa.

Wote hao hawakupenda majina yao yatajwe.Walisema mambo yafuatayo Rais ayaangalie kwa ukaribu:-
  • Kudhibiti mfumuko wa bei za bidhaa mbambali zikiwemo vyakula,vifaa vya ujenzi na vitu vingi wameviainisha katika maoni yao.
  • kero za vijana na hatima yao,wapewe mikopo ipitie ngazi za chini kwenye serikali za vijiji na mitaa,kisha ifuatiliwe Isiwe kama faidika  na mapesa ya kikwete kupitia Benki ya NMB.walinufaika wajanja wachache wenye dhiki walizisikia redioni.
  • Rais awe mkali kwa mambo yanayo tekelezwa na watendaji wake bila viwango kwa jina jinine kuchakachuliwa.Asiwaone haya wanavuruga mipangilio aliyoiweka kwa ajili ya kumletea mwananchi maendeleo.Asiwachekee wanaotaka kuvuruga wananchi kwa kutumia maandamano yenye picha za kisiasa ndani yake.
  • Watendaji wasio kidhi viwango waondolewe madarakani awateuliwe wengine kulinda heshima ya nchi na Taifa kwa uju,mla.
  • Matendo yawe mengi zaidi kuliko maneno katika ngazi zote za uongozi.Na Rais afuatilie ili kudhibiti mianya ya uzembe kwa watendaji wake ,akifanya hivyo kutaondoa hata maswali tata kutoka vyama pinzani..kwani wapinzani  wao hawaoni hata moja jema lililo fanywa na Chama Tawala tangu Uhuru.

No comments:

Post a Comment