Sunday, March 6, 2011

NI MAMBO YA DUNIA SAYARI YENYE UHAI KWA UUMBAJI WA MUNGU BINADAMU KAAMBULIA KUTENGENEZA VITU.

Dunia ni matokeo ya uumbaji wa Mungu,ambayo viumbe vyote vimo ndani yake,vyenye uhai na visivyo na uhai.Lakini kuna Tafsiri nyingi zilizotolewa na Maandiko mbalimbali ya vitabu vya Dini,na wanasayansi katika kuielazea Dunia.


DUNIA ni moja wapo ya sayari ambayo iliyokamatia uhai wa viumbe vyenye uhai na vitu visivyo na uhai.Na kubwa zaidi kuna binadamu ambaye aliambiwa na Mungu avitawale vitu vyote vilivyomo katika Dunia,kwa kuwa kapewa akili na utashi.

Kwenye ardhi viumbe hai ni vingi ambavyo tunaamini wanasanyansi wameshavibaisha kwa mamilioni yake, wanyama kwa makundi yake,ndege warukao na wale wasio na uwezo wa kuruka kutokana na uzito wao kama mbuni,kuna mimea,kuna miamba,kuna maji ambayo yameitwa bahari,mito,mabwawa,chemichemi.

Sifa za dunia kuwa na majira mbalimbali katika mwaka,kutokana na kuinama kwake kwa digrii 23.5.Hilo hufanya kuwe na viwango mbalimbali vya hali ya hewa joto au baridi.Mwinamo wake katika mhimili wake umeonekana kuwa bora kabisa,ili kuendeleza uhai.

Je ni kweli Dunia inamzingo wakilometa 40,000 na inazunguka mara moja kila saa 24.?
Je maeneo maeneo yaliyo kwenye Ikweta au karibu yanasonga kwa kilometa 1,600 hivi kwa saa?
Ni kweli Dunia inazunguka jua kwa kilometa 30 hivi kwa sekunde? Ambapo mfumo wa jua kwa ujumla unazunguka kitovu cha kilimia kwa mwendo wenye kustaajabisha kwa kilometa 249 kwa sekunde.Je unaweza kulinganisha na risasi inayosafiri kwa mwendo unaopungua kilomita mbili kwa sekunde?

Hayo mambo ya Sayari ambazo ni kazi ya Mungu,aliye umba mbigu na Dunia na ndani ya Dunia hiyo kaumba vumbe vyenye uhai na visivyo na uhai.Ambapo kamuumba Binadamu  atawale vitu hivyo vya nchi kavu na vya majini.Baadhi ya Binadamu hao ndio wanasayansi ,walijaribu kubuni vitu mbalimbali na wakaweza ila wakashindwa kumtengeneza binadamu mwenzao ambaye angefanana na wao,Unadhani kuna siku huyu binadamu anaweza kuumba binadamu mwenziwe?.

No comments:

Post a Comment