Friday, March 25, 2011

USHURU WA WAENDESHA PIKIPIKI HALMASHAURI YA MANISPAA YA SONGEA SASA UMEZIDI


Waendesha pikipiki kwa jina maarufu mjini hapa Songea Yebo yebo wameulalamikia uongozi wa Manispaa ya Songea kitendo cha kutangaza kuwa waendesha Yebo yebo walipe ushuru wa shilingi 30,000 baada ya miezi sita na siku ya tatu yake waanze kukamata wale wote wasio tekeleza agizo hilo.


Wandesha yebo yebo hizo wanasema wanalipa BIMA shilingi  25,000 kwa mwaka,TRA shiligi 95,000 kwa mwaka na kisha tena shilingi 30,000 kila baada ya miezi 6kwenye manispaa, wanasema hakuna faida yoyote kutokana na kuwa na utitiri wa yebo yebo katika manispaa hiyo.

No comments:

Post a Comment