Thursday, March 17, 2011

MBINGA NA ELIMU YA SEKONDARI WALIVYO PANIA KUBORESHA MAZINGIRA YA KUTOLEA ELIMU



 

Wilaya ya Mbinga imeweka  mikakati ya kuinua kiwango cha taaluma ya  elimu ya sekondari ambapo wilaya ina  shule za sekondari 60 kati yake shule 51 zinamilikiwa na serikali na Halmashauri, na 9 zinamilikiwa na mashirika ya dini na watu binafsi.

Kwa mujibu wa taarifa ya kutathmini elimu ya wilaya hiyo inaonyesha kuwa wilaya ina wanafunzi 23,140 kati yao wavulana 12,003 na wasichana 11,137.katika idadi hiyo wanafunzi walemavu wa aina mbalimbali 103 kati yao wavulana 57 na wasichana 46.

Aidha wilaya bado una changamoto kadhaa zikiwemo za upungifu wa walimu 267 kati ya walimu 726 wanaohitajika katika shule hizo za sekondari zenye walimu 459 wakiwemo wanaume 349 na wanawake 110.



No comments:

Post a Comment