Monday, March 14, 2011

MATOKEO YA KILIMO KWANZA MKOANI RUVUMA MAHINDI YANALALIANA BOHARI YA KUHIDHAFI MAHINDI

Kilimo Kwanza imeonyesha mafanikio makubwa sana kwa walanguzi wa mahindi waliokwenda kununua mahindi huko huko vijijini kwa bei ya hasara,kisha kuyauza kwa faida wakimwacha mkulima hana kitu.

Serikali imenunua mahindi hadi msimu wa kununu mahindi hayo umekwisha na mahindi bado wananchi wanayo vijijini,ambayo yanakutana na mahindi yaliyokuwepo shambani,hata kwenye hifadhi ya taifa Luhuwiko bado kuna mahindi ya mwaka juzi,mwaka jana na mengine  bado yako shamba.

Serikali iangalie uwezekano wa kuyasomba mahindi hayo wapelekewe wenye shida ya chakula,pia wakulima watafutiwe soko la kuuzia mahindi yao baada ya mavuno,kwani walanguzi bado wanawalalia wakulima.

No comments:

Post a Comment