Sunday, May 15, 2011

KIFO HAKINA UPENDO MTU AKIFA BASI UPENDO HAUPO TENA ANAOGOPWA FATHER MALENDA ANAELEZEA


Sikiliza mkasa huu anauelezea Padre Basley Malenda.

Kijana mmoja jina lake hakulitaja alipendwa sana na wazazi wake,pia yeye aliwapenda wazazi wake kila walicho mwambia alikitii.Lakini kijana huyo alitaka kuingia kwenye wito wa Upadre.Akawaambia wazazi wake azma yake hapo baadaye.

Wazazi hawakuwa tayari kumruhusu ila walimtafutia mchumba mzuri sana,na mchumba naye alimpenda sana kijana,akawa anafika kumfulia nguo,kumpikia,ila kijana bado alisikia wito unamwita.

Kijana aliamua kwenda kwa Padre amweleze yanayo mtatiza,Padre akamuuliza ni kweli wanakupenda hao,kijana akajibu ndiyo.Padre alimwambia aende nyumbani,basi yule Padre alisali pale muda kidogo kilio kilisikika kwa yule mzee kuwa kijana amekufa.
Basi walipo peleka kuzika padre yuleyule alisalia maiti,kisha akawambia waingize mwili kaburini,yule binti naye akaingia kwa uchungu kuwa anampenda sana,mara mtu mmoja akasema mfukieni nay eye,Binti aliruka kuwa haiwezekani.

Basi padre akawaambia toeni mwili nje ya kaburi,akamuuliza mama mzazi kuwa uko tayari kijana wako awemzima maana nina uwezo kwa kumfanya awe hai.yule mama alisema hapana nitamzaa mwingine.Baba naye alipo ulizwa alisema huyu kafa basi tutatafuta motto mweingine.

Zamu ikafika kwa mchumba akaulizwa kama mchumba wake akiwa hai atakuwa tayari kuwa naye? Mchumba alisema mbona wanaume wako wengi.Basi aliwambia waliofunga sanduku walifungue.kijana akaamka kisha padre alimuuliza kuwa kama huko ulikokuwa alisikia baba ,mama na mchumba wake walivyokuwa wakisema,alisema niliwasikia wote.

Ndipo yule alipogungua kumbe hakuna upendo wa dhati miongoni mwa binadamu, binadamu na kifo,wanasema kwa nje tu maoyoni hakuna.Ndipo Padre Malenda aliposema mototo kama anawito wa upadre mruhusu akaitikie wito kwa aliye mwita kuwa mchungaji wa konddo zake.

No comments:

Post a Comment