Saturday, May 7, 2011

Kigonsera na Songea Boys kupewa 100 M/- za ukarabati




SHULE kongwe za Kigonsera ya Songea boys zitapewa shilingi 100,000,000  na serikali kwa ajili ya ukarabati wa majengo na miundombinu,ambapo shule ya wasichana ya Songea imeshapewa sh.50,000,000 wanachotakiwa warudishe mchanganuo wa matumizi wapewe nyingine.

Hayo yamaesemwa na Naibu Waziri wa Nchi Elimu TAMISEMI Mhe.Kassim Majaliwa wakati wa majumuisho ya ziara yake ya siku sita mkoani Ruvuma katika ukumbi wa songea Club hapo jana.

Mh.Majaliwa alisema kila shule italetewa shilingi 50,000,000 ila kwa shule ya sekondari ya Kigonsera fedha hizo wazitumie kwa kununulia jenereta kubwa lenge uwezo wa kufua umeme wakusambaza  shuleni hapo.

Sambamba na hilo waziri alisema kuna upungufu wa walimu 40,000 wa shule za sekondari na 179,000 wa shule za msingi nchini.ambapo pengo hilo litazibwa hivi karibuni kwakuwa walimu wa stashahada na shahada watamaliza mwaka huu na mwakani.

No comments:

Post a Comment