Friday, May 13, 2011

LEO SIKUONEKANA KWENYE BLOG NI KWA SABABU YA KUCHEZA NA MTANDAO AKANIFUNGIA

Samahani wanablogger wenzangu  kwa kutoonekana hewani  kwa sababu ya mainjinia wa Google walivyo nifanyia roho mbaya.Lakini si haba tuko nanyi tena.0756-282320,0652- 828964,0778-836662

2 comments:

  1. Hi Chris,
    Si wewe uliyefungiwa kwa makusudi, bali lilikuwa ni tatizo la Blogger duniani kote. Wenye blogu karibu wote walikumbwa na taharuki hadi hapo baadaye mambo yaliporekebishwa, hivyo usijisikie vibaya ukaona umwakuwa singled out. Pole kwa usumbufu!

    Nashukuru kwa taarifa na habari unazotupatia!

    ReplyDelete
  2. Ni kweli, kwa siku yapata mbili hivi blogu zetu zimekwama. Mwanzoni sikujua, hadi nilipoangalia kwa makini tangazo la wenye kuendesha hii mitambo.

    Leo mambo yamerudia hali ya kawaida, lakini nimeona kwenye posti yangu kuhusu mpiga debe wangu, maoni aliyotoa Mzee Sikapundwa na majibu yangu, yameyeyuka, yaani hayaonekani tena pale kwenye sehemu ya maoni.

    Hali hii iliyotokea inatuonyesha wazi madhara ya kuwategemea wengine. Na papo hapo, kwa jinsi dunia ilivyokosa usawa, sisi tutabaki kuwa mateka kwa hao wenye uwezo wa kumiliki na kuendesha mitambo hii, kama vile tunavyoendelea kuwa mateka katika mfumo wa kibepari wa kimataifa.

    Sijui tutajikwamuaje, hasa katika dunia hii ya utandawazi wa leo, utandawazi ambao unaigeuza dunia kuwa kijiji.

    ReplyDelete