Tuesday, June 28, 2011

BREAKING NEWS ! Mikataba ya madini iangaliwe upya ili mwananchi anufaike na rasilimali yake



Viongozi wa madhehebu ya dini mbalimbali nchini wameitaka serikali kuangalia upya mikataba ya madini iliyo wekwa awali ambayo haimsaidii mwananchi kutokana na mapato yatokanayo na madini hayo,badala yake huambulia kuona mashimo tu maeneo yanapochimbwa madini hayo.

Tamko la pamoja la viongozi hao wa madhehebu ya dini nchini lilitolewa na Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT ) ,Baraza la Maaskofu katoliki  Tanzania ( TEC ) na Baraza kuu la Waislamu Tanzania ( BAKWATA ),wote kwa pamoja waliitaka serikali kutazama upya mikataba ya madini kwa wawekezaji wa nje.

Aidha Viongozi hao walitamka hayo hivi karibuni kuwa haki ya kikatiba haikuzingatiwa kwenye mikataba hiyo ya madini, hivyo katiba haina budi kuandikwa upya ili maslahi ya pande zote yazingatiwe.

Walisema haki za binadamu katika maeneo  ya migodi haipo,haki za binadamu si suala la kisiasa,kama kuna raia amefanya makosa hatua stahiki za kisheria zichukuliwe,sio vyombo vya sheria  vinaibuka na kuanza kuhatarisha amani kwa raia wake.

Walisema athari zilizopo katika sekta ya madini zisipotatuliwa mapema ni hatari kwa umoja wa Taifa ( Source Mwananchi Juni 25 mwaka huu )

No comments:

Post a Comment