Wednesday, August 31, 2011

VIONGOZI WA MADHEHEBU YA DINI WATAKIWA KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KATIKA KUKEMEA MATENDO MAOVU



RAIS Jakaya Kikwete amewataka viongozi wa madhehebu ya dini nchini kishirikana na serikali katika kukemea maovu yakiwemo ya biashara ya madawa ya kulevya ambayo yana haribu vijina ,pia wanafunzi wa shule za msingu,sekondari amabo ndiyo nguvu kazi ya Taifa.
Rais Kikwete alisema hayo katika hotuba yake aliyoitoa kwenye Baraza la Eid iliyofanyika  kitaifa katika Msikiti wa Mkoa wa Dodoma leo akiwa mgeni rasmi katika sherehe hizo za Eid,l alisisitiza kuwa ni wajibu wake kukemea,kuonya na kutahadharisha hatari itakayo kuja mbele yake.
Alisema kuwa tahadhari hiyo aliitoa siku ya kumweka wakfu askofu Jonh Ndimbo wa jimbo la Mbinga kuwa baadhi ya viongozi wa dini wanajihusisha na madawa ya kulevywa na wengine walishikwa,wakiwemo watoto wa viongozi wa madhehebu ya dini.’Ilikuwa ni wajibu wangu kukemea na tahadharisha wimbi la bishara ya madawa hayo kuingia katika madhehebu ya dini’ alisisitiza Rais.
‘Viongozi wa madhehebu ya dini zote tushirikiane katika mapambano haya ya kukemea maovu yanayo sababishwa na biashara hii.’ Alisema Rais.Hili ni tatizo kubwa tunaomba tushirikiane alisisitiza tena Rais.
Aidha katika Baraza hilo la Eid Rais alisema kuwa Serikali ina Mahakama yake hivyo haiwezi kuunda mahakama nyingine,alipokuwa akiwaeleza Waislamu kuwa jambo la Mahakama ya kadhi  bado linaendelea,anashughulikia Waziri mkuu ,wala hakuna mkono wa mtu.
Alisema suala hilo litajadiliwa Bungeni,na Bungeni hakuna siri,kila mmoja atakuwa na nafasi yake ya kuchangia suala hilo,wala siyo shinikizo la Baraza la Maskofu ila wao walicho kisema nikuwa suala hilo liachiwe kwa waislamu wenyewe na siyo serikali kuingilia musuala ya kidini.
Alisema lengo la mahakama hiyo ni kwa ajili ya Talaka,Mirathi na wafu,si zaidi ya hayo masuala yote yakijinai,madai,wizi yaachiwe kwenye mahakama ya serikali na siyo mahama ya kadhi.

No comments:

Post a Comment