Sunday, August 14, 2011

BIBI ERIKA KAZI ULAYA AOMBA MSAADA KUTOKA KWA WASAMARIA WEMA KUTUNZA WATOTO YATIMA HANGA KATI WILAYANI NAMTUMBO MOA WA RUVUMA.

 Bibi Erika Kaziulaya anayewatunza watoto yatima ( Orphans ) Kijiji cha Hanga kati wilaya ya Namtumbo Mkoani Ruvuma anawatunza watoto hao na kuwasomesha shule za msingi,sekondari hadi chuo kikuu,ameelemewa baada ya kuishiwa fedha ( fund )
 Mama huyu ni shuhuda wa kijiji hicho  anacho lelea watoto hao yatima Bibi kazi Ulaya
 Bibi kazi Ulaya
 Baadhi ya wanafunzi ( watoto  yatima ) ambao Bibi kazi ulaya anawalea na kuwasomesha
Mwenye kiti wa kijiji hicho cha Hanga kati akimweleza ripota aliyetembelea kituo hicho cha kulelea watoto yatima cha Bibi Kazi Ulaya Hanga kati.Anasema kama Bibi kazi Ualaya amezidiwa kwa kukosa fedha za kuwalea watoto hao na kuwasomesha.hivyo anaiomba serikali kupitia wizara ya Maendeleo,wafadhili mbali mbali,wazazi na walezi pamoja na mashirika yasiyo ya kiserikali kumsaidia Bibi huyo Mjane aliyejitolea kwa nguvu zake kuwakusanya watoto yatima kuwalea na kuwasomesha hadi chuo kikuu.


AITWA OMBA OMBA BIBI ERIKA  KAZI  ULYA BAADA KUELEMEWA NA  MZIGO WA KUWALEA  WATOTO YATIMA NA KUWASOMESHA KWA GHARAMA ZAKE WENYEWE

Bibi Erika Kaziulaya ni mstaafu wa chuoa cha ualimu Songea ambapo alifanya kazi kwa miaka 33,hatimaye akaitwa na Mungu kuwa mlezi wa watoto yatima kijiji cha Hanga kati wilaya ya Nantumbo mkoa wa Ruvuma.

Bibi kaziulaya analeya watoto yatima waliyofiwa na wazazi wao,kwa  mara yakwanza watoto hao wakiwapeleka katika nyumba yake yakuwalea,wanakataa na kuogopa kwa kuwa labda wametokea kwenye mazingirz ya kunyanyasika na kufanyiwa ukatili,lakini baada ya muda wanazoea.

Bibi Kaziulaya aliyefiwa na Mumewe anawalea watoto hao na kuwa somesha ambapo kati yao mmoja anasoma chuo kikuu cha Tumaini mwaka wa kwanza na wengine 20 wanasoma sekondari na seminari na anawagharimia mwenyewe kwa fedha za kinua mgongo ambazo sasa zimemalizika.

Alisema kuna wengine wanasoma shule za msingi.Alisema kuna kundi lingine walio maliza sekondari na wakashindwa katika mitihani yao ya taifa,hawa anawafundisha ushonaji.

Anasema amenunuvyerehani na mwalimu mmoja anawafundisha hapo tanyumbani kwa miaka miwili ( 2 ) baadaye wataenda kusoma tena Hanga kwa miaka mingie miwili ( 2 ) ambapo watafanya mitihani ya VETA kisha watajiajiri wenyewe.

Aidha Bibi Kaziulaya anaiomba serikali imlipe kinua mgongo alichofundisha kwa miezi 9 ili aweze kuwalipia ada baadhi ya watoto hao yatima wanaosoma sekondari na seminari na matumizi kwa huyo wa chuo kikuu.

Any body can assist Mrs. Kaziulaya  anything which you think it help her in supporting those Orphans in school fees, food, soap, sugar, vegetable anywhere you are please help this women engaged in orphans help without enough  fund using her won source of income.’

Ukweli mama huyo anaomba msaada waina yoyote,ikiwa fedha,chakula ,maji,sabuni,nguo,matandiko,madawa,vitanda.kutoka kwa serikali,wazazi na walezi na wafadhili wa ndani na nje.mawasiliani kupitia TBC Kanda ya Ziwa Nyasa,Blog hii kwa e- mail christiansikapundwa@yahoo.com au +225756 -282369. ili kuwasiliana na Bibi Kaziulaya.

Ni moyo wa pekee kulea watoto wa watu ambao hana mahusiano nao kiudugu wala hana mfadhili yeyote anayemsaidia.kwa hiyo kutoa ni moyo humsaidii Bibi huyo,bali ni kuwasaidia watoto hawa waliyopoteza wazazi wao.

No comments:

Post a Comment