Sunday, August 14, 2011

Breaking News Dkt Asha Rozi Migiro kuzindua Taarifa ya Utafiti dhidi ya ukatili kwa mtoto Jijini Dar es salaam

 Dkt Ashibu Rozi Migiro Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Matifa akiongea kabla ya kuzindua Ripoti ya Utafiti wa Ukatili dhidi ya mtoto Jijini Dar es salaam nchini Tanzania.
 Mheshimiwa sophia Simba Mbunge akimkaribisha naibu katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Dkt Asha Rozi Migiro Jijini Dar es salaam hivi karibuni.


Naibu katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa wakati wa uzinduzi wa ripoti ya utafiti wa ukatili dhidi ya mtoto Jijini Dar es salaam

Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Dkt Asha Rozi Migiro alisema hayo wakati wa uzinduzi wa ripoti ya utafiti wa ukatili zidi ya watoto,Jijini Dar es salaam.

Dkt.Migiro alisema nusu ya wanzania ni watoto kama watafanyiwa ukatili watoto watakuwa hawamwamini mtu kwa kujua ni mkatili,na kuwa na taifa la watu wakatili hapo baadaye.

Alisema uzinduzi wa utafiti juu ya ukatili kwa watoto kumeandika historia Afrika kwa serikali ya Tanzania kuridhia utafiti huu kufanyika.Alisema watoto wanafanyiwa vitendo vya ukatili mbalimbali.

Alivitaja ingawa si vyote kuwa ni pamoja na kupigwa,kubakwa na kunajisiwa,kubebeshwa mizigo,kufanywa kazi kwenye migodi kupewa mamba wakiwa na umri mdogo.

Aidha alisema Umoja wa Mataifa unianza utafiti huu wa ukatili zidi ya watoto mwaka 1990 na Tanzania ikaridhia kufanya utafiti na kupata ripotia,ambapo leoumezinduliwa na Dkt Asha Rozi Migiro.

Alisema ripoti ya utafiti huu imeonyesha kuna mambo mengi ambayo watoto wanafanyiwa ukatili,ubakaji na unajisi unaweza kumpatia mwathirika magonjwa yakiwemo  ya Virusi vya UKIMWI na UKIMWI wenyewe na magonjwa ya zinaa.

Alisema taasisi za kidini na vyombo vya sheria vikiungana kumsaidia motto dhidi ya ukatili vitendo hivyo vitapungua,wazazi,mahakama na polisi wakiwa na mshikamano wa kutosha mototo ataweza kuishi kwa amani kwa kuwa anajua atalindwa na kuwa huru kujieleza pale apatapo matatizo.

No comments:

Post a Comment