Monday, May 28, 2012

MWENGE WA UHURU MKOANI RUVUMA UTAFANYA KAZI YA KUKAGUA MIRADI 51 YENYE GHARAMA YA TSHS,1,930,357,902.



Gharama hiyo yenye mchanganuo wa uchangiaji wa gharama za miradi ya Mwenge wa Uhuru kwa mwaka  2012 ni kama ifuatavyo:-
  • Nguvu za wananchi Tshs.296,022,645/=
  • Halmashauri za wilaya na Manispaa Tshs.204,486,125/=
  • Serikali Kuu Tshs.773,599,581
  • Wadau wa Maendeleo Tshs.458,809,551/=
  • Watu Binafsi Tshs.287,440,000/=
Mwenge uko Mkoani Ruvuma Umepokelewa leo na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma kutoka Mkoa wa Njombe katika Wilaya ya Nyasa na  kuanza kukimbizwa katika wilaya zote tano zenye Halmashauri sita ambazo ni Wilaya ya Nyasa, Mbinga, Songea, Namtumbo na Tunduru.
    Ukiwa Mkoani Ruvuma Mwenge wa Uhuru utafanya kazi ya kufungua miradi 13 yenye thamani ya Tshs.390,684,832 kuweka mawe ya msingi miradi 22 yenye thamani ya Tshs.1,303,187,695, kuzindua miradi 12 yenye thamani ya Tshs.141,045,375 na miradi 04 yenye thamani ya Tshs.34,840,000 itakaguliwa na kufanya jumla ya miradi yote kuwa 51 yenye thamani ya Tshs.1,930,357,902.
Baba wa Taifa mwalimu Julius Kambarage Nyerere alisema “Sisi tunataka kuwasha Mwenge na kuuweka juu ya mlima Kilimanjaro umulike hata nje ya mipaka yetu, ulete tumaini pale ambapo hakuna matumaini, upendo mahali palipo na chuki na heshima palipojaa dharau”.
Mwenge umekuwa ni kichocheo kikubwa cha shughuli za maendeleo, umoja, mshikamano na amani kwa Taifa letu.Lakini usemi wa Baba wa Taifa unaanza kuingia dosari Amani hiyo inaanza kutoweka,unasikia wenzetu Zanzibar Makanisa yanachomwa,tatizo hawataki Muungano sasa kukataa Mungano kuna uhusiano gani na Kuchoma makanisa ? Tunaelekea wapi sasa.



No comments:

Post a Comment