Tuesday, May 1, 2012

MEI MOSI MKUU WA MKOA WA RUVUMA BWANA SAID THABIT MWAMBUNGU AWATAKA WAAAJIRI WASIZALISHE MADENI YASIYO YA LAZIMA

 Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Bwana Said Thabiti Mwambungu akihutumia wananchi katika uwanja wa majimaji mjini Songea siku ya Mei Mosi leo.

 Baadhi ya viongozi waliyoandamana na Mkuu wa Mkoa.
Baadhi ya viongizi waliyoa andamana na mkuu wa mkoa wa Ruvuma leo Mei Mosi uwanja wa majimaji Mjini Songea



BWANA Mwambungu alisema hayo leo kwenye maadhimisho Mei Mosi inayoa adhimishwa duniani kote,katika uwanja wa majimaji mjini Songea ,akihutubia maelfu ya wqafanya kazi ambao kati yao 160 walitunukiwa fedha na vyeti kwa utendaji bora wao wa kazi.
Aidha mkuu huyo ametoa wito kwa viongozi wa dini,viongozi waina zote kuhamasisha wananchi kujitokeza kutoa maoni yao wakati wajumbe wa Tume ya katiba mpya watakapo wasili.
Ameongezea pia kuwa sambamba na kuhamasisha wananchi bila ya kujali itikadi za vyama vyo kujitokeza katika sensa ya kuhesabu watu itakayofanyika mwaka huu nchi nzima.
Alisema sensa ni uti wa mgongo wa maendeleo ya uchumi wa taifa,hivyo ni vyema watu watimize wajibu wao katika sensa ya kujua idadi ya watu ili serikali iweze kupanga shughuli zake za maendeleo kwa wananchi wake.
Mei mosi kwa kawaida wafanya kazi pamoja na kupewa tuzo lakini pia wanamatarajio makubwa ya kusikia serikali kupandisha viwango vya mishahara kwa watumishi wake ingawa hakitoshelezi malengo ya kila mmoja.

No comments:

Post a Comment