Saturday, May 5, 2012

MAWAZIRI HAWAWEZI KUWAJIBIKA PEKEYAO BALI NI PAMOJA , NA WATENDAJI WAO WATAHUSIKA PIA- KIKWETE


MAWAZIRI waliyo wajibika kutokana na utendaji mbovu wa majukumu yao,hawawezi kuwajibishwa peke yao,ni pamoja na watendaji wao wakiwemo makatibu wakuu wao,wakurugenzi,viongozi wa mashirika ya Umma kama wamo katika mkumbo huo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete alisema hayo kwa wananchi kupitia vyombo vya habari Ikulu Jijini Dar es salaam jana  kabla ya kutangaza Baraza lake jipya la mawaziri.

Alesema inawezeka kuna baadhi ya Mawaziri hakuhusika na lolote ila ni kwa sababu ya watendaji wao kwa lengo kukomoana,havyo vitendo hivyo haviwezi kuvumilika ni budi na wao wahusike kwa hili.

Kwa maoni mbali mbali ya wakazi wa Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma wamemsifia sana Rais Kikwete kwa uamuzi aliyo uchukua wa kubadilisha mawaziri na wengine wapya kuingia na wabovu kutolewa,hiyo ndiyo Demokrasi walisema watoa maoni hao,’Ni baraza safi kama watatekeleza yale watakayo agizwa’.walisema.( Source TBC )

No comments:

Post a Comment