Thursday, May 31, 2012

MAPENZI YA SABABISHA MTOTO MLEMAVU KUAWA NA KUTUPWA MTONI SONGEA

Aliyekuwa Kamanda wa Polisi mkoani Ruvuma ( RPC ) Michael Kamuhanda anayehamia Mkoa wa Iringa baada ya kuongea na waandishi wa habari mkoani hapa leo katika kumtambulishi Kamanda mgeni wa mkoa huo ( RPC ) aliyehamishiwa hivi karibuni ACP Deusdedit Nsemike hayupo pichani..

MTOTO mwenye umri wa mwaka mmoja na miezi mitatu auawa na bwana wa mama mwenye mtoto Rebeka Cheni na kutupwa mtoni,Kamanda wa Mkoa wa Ruvuma anaehamia mkoa wa Iringa  Michael Kamuhanda leo amewaambia waandihi wa habari kuwa chanzo ya mauaji ya mtoto huyo ni mapenzi.
Alisema kuwa inasemekana kuwa mama wa mtoto huyo aliambiwa na bwana ambaye hakuzaa naye mtoto huyo kuwa wamuue ili waendelee na mapenzi yao kwa raha kwani mtoto huyo alikuwa mlemavu wa akili Tahira,ndipo mama huyo alivyo toka nje na kumwacha mwanae ndani,muda huo bwana huyo mkatili alivyo pata mwanya wa kummaliza mtoto Rebeka.
 Alisema baada ya kufanya kitendo hicho watuhumiwa walichukua mwili wa mtoto huyo na kuitupa mtoni,wasamaria weme walivyo kundua hilo waliitaarifu polisi.Na kwamba wote wako mikononi mwa polisi na upelelezi unaendelea.

No comments:

Post a Comment