Thursday, May 31, 2012

KAMANDA WA POLISI ( RPC ) MGENI ACP DEUSDEDITH NSEMIKE MKOANI RUVUMA ATABULISHWA KWA WAANDISHI WA HABARI LEO.NA AKAMANDA WA ZAMANI ANAYE HAMISHIWA MKOANI INGA MICHAEL KAMUHANDA

 Kamanda mgeni wa polisi RPC Mkoani Ruvuma ACP  Deusdedit Nsemike  baada ya kutambulishwa kwa waandishi wa habari wa mkoa wa Ruvuma leo

 picha ya pamoja na waandishi wa habari wa Ruvuma leo baada ya utambulisho wa RPC Mgeni nje ya jengo la polisi mkoa mjini Songea Kamanda mgeni  Deusdedit Nsemike wa tatu kutoka kushoto.

Bwana Juma Nyuamayo wakizungumza na rpc Michael Kamuhanda leo.
.
KAMANDA wa Polisi (RPC) Mgeni ACP Deusdedith Nsemike Leo ametambuliwa kwa waandishi wa habari wa Mkoa wa Ruvuma katika ukumbi wa Jengo la Polisi mkoani na Kamanda Michael Kamuhanda anaye hamishiwa mkoa wa Iringa.
  Kamanda Nsemike alisema kuwa atakuwa tayari kufanya kazi na waandishi wa habari,kwani nimuwazi,na kwamba anaomba ushirikiano wa kutosha kutoka kwa waandishi hao japo watapata jambo ambalo ni la uhalifu.
  Aidha alisema kuwa atahitaji utii  wa sheria bila masharti,Mahusiano pamoja na Idara nyingine zikiwemo za Ustawi wa jamii,Elimu,Afya ,michezo na Halmashauri za Wilaya.
  Vilevile alisema kuwa atahitaji ushirikiano na viongozi wa ulinzi na usalama ili kuhakikisha Falsafa ya Polisi Jamii inatekelezwa kwa kiwango cha juu kwa kuzingatia sheria za nchi.
   Alisema kuwa iwapo wananchi watapata taarifa za fujo,ujambazi,zitaarifiwe mapema katika vyombo vinavyohusika kabla hakujatokea madhara makubwa.
Awali kamanda Michael Kamuhanda aliwaonba waandishi wa habari hao kuwa na ushirikiano wa karibu na Kamanda Nsemike kama vile alivyopata ushirikiano yeye katika kufanikisha shughuli zake za ulinzi na usalama katika Mkoa wa Ruvuma.
Pia akamweleza Kamanda huyo mgeni Mkoani hapa kuwa asiwe na mashaka na waandishi wa mkoa huo katika utendaji wao wa kazi.
Kamanda wa Polisi Mkoani Ruvuma Michael Kamuhanda amepata uhamisho kwenda Mkoa wa Iringa, Ni matumaini ya waandishi wa Mkoa wa Iringa watampa ushirikiano wa kutosha Kamuhanda katika shughuli zake,kwani wanahabari ni kioo cha Jamii

No comments:

Post a Comment