Friday, February 24, 2012

WAENDESHA PIKIPIKI KATIKA MANISPAA YA SONGEA SASA KUVAA SARE

 Madereve wa yeboyebo kabla ya kuongea na mkuu wa mkoa wa Ruvuma Bwana Said Thabit Mwambungu kwenye ukumbi wa Songea Club.
 Baadhi ya viongozu ,wamiliki na waendesha pikipiki katika ukumbi wa Songea Club wakimsubili mkuu wa mkoa mjini Songea.
 Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Bw.Said Thabit Mwambungu akiongea na madereva wa yeboyebo na wamiliki wa yeboyebo hizo katika ukumbi wa Songea Club jana.
 Mkuu wa Wilaya ya Songea Bwana Ole Thomas Sabaya  kisisitiza umuhimu wa kuwa na sare wakati wa kuendesha yeboyebo hizo.
Bw.Mwambungu akishikana mikono na madereva hao baada ya kikao Songea Club jana.



Madereva wa Yebo yebo Songea waandaliwa sare

  • Zenye namba na sehemu anakotoka
  • Ziweze kumtambulisha kiurahisi

MADEREVA yeboyebo katika Manispaa ya Songea wanaandaliwa sare ambazo zitasaidia kumtambua mwendesha pikipiki kuwa ni wa eneo gain,endapo akapatwa na matatizo na mteja wake itakuwa ni rahisi kufuatilia.

Mkuu wa mkoa wa Ruvuma alisema hayo katika ukumbi wa Songea Club jan alipokuwa akizungumza na wamiliki na waendesha pikipiki wa mjini Songea,ambao hawakuweza kufika wote kwenye mkutano huo baada ya wengine kwenda Litola kumzika mwendesha pikipiki mwenzao.
Aidha Bw.Mwambungu aliwaomba waendesha pikipiki hao kuwa makini wakati wa chukua abiria wao kwakuwa abiria wengine si wazuri kwa uhai wao,na kwamba  kazi yao nzuri lakini ikawa mbaya   katika maisha yao kutokana na abiria wanaowachukua hasa ikiwa zaidi ya mmoja.
Alisema kuwa waachane na ushabiki ambao unaweza  ukaleta madhara makubwa katika Jamii kama ilivyo jitokeza katika maandamano waliyoyafanya kwa kuwatupia mawe polisi,ofisi ya CCM mkoa na wilaya,mkuu wa mkoa,Ikulu ndogo na Songea Club kuliko sababisha Jeshi Polisi  jibu kwa piga mabomu ya machozi na silaha za moto.

No comments:

Post a Comment