Monday, February 13, 2012

KUNGURU WEUSI UNAIJUA HISTIRIA YAO ? INASEMEKANI KUWA KUNA MTAALAMU MMOJA ALIDAI KUWA KUNGURU HAO WALITOLEWA NCHINI INDIA MIAKA YA 1895 KUPELEKWA MJI MKONGWE ZANZIBAR ILI KUPUNGUZA UCHAFU



MTAALAMU huyo alisema kuwa enzi hizo za utawala wa kigeni Zanzibar ulikerwa na uchafu katika mji Mkongwe,hivyo waliamua kuwambia watawala wenzao walioko India wawaletee kunguru hao ili wasaidie kupunguza uchafu.

Kutoka miaka hiyo kunguru hao wakawa wengi Zanzibar,wakiwa wakisaidia kuondoa uchafu siyo mji Mkongwe peke yake bali Zanzibar yote,Kunguru hao wamekuwa kero,wanasababisha kuchafua mazingira kutokana na kula kila kitu wanacho kiona.na kukiacha hapo na kuondoka zake.

Isitoshe kunguru hao sasa wamekuwa kero pia katika Jiji la Dar es Salaam,Mhimbili,Osheni Road,Temeke,Fery  na maeneo yote yenye dalili ya vyakula.Kunguru wale sio waoga kamwe wako tayari kuchukua nyama au samaki zilizoanikwa mbele ya mwenye samaki au nyama yake.

Aidha kunguru hao wanauwezo mkubwa wa kusambaza vimelea vya maradhi,kwakuwa wanaweza kutoka kula mzoga, na hatimaye wakatua kwenye vyakula vya watu na kuacha vimelea vya maradhi kwenye chakula kile. Je habari hizo ni za kweli? Kwamba kunguru hao walichukuliwa India ? waliletwa kanguru au mayai yao, na kweli wanakera ?

Kuhusu kunguru je wale wenye baka jeupe wao hawasumbui isipokuwa kunguru weusi pekee ? Mwaka Fulani nilikuwa Ward ya Mwaisela Muhimbili Jijini Dar es Salaam,kwenye corridor kunguru mwenye baka jeupe alikwapua vipande vya mikate ya wagonjwa kwenye kigari alichokuwa akikisukuma muuguzi mbele yake alipotaka kuingiza ndani .

Kama kweli wanakera na wanaleta madhara kwa afya ya binadamu,sasa kifanyike nini kuwapunguza kunguru wote weusi na wenye baka jeupe,kwani kunguru wamezagaa Tanzania nzima hasa wale wenye baka jeupe.

No comments:

Post a Comment