Tuesday, February 28, 2012

TAMASHA LA MAKUMBUSHO YA TAIFA YA MAJIMAJI JANA YAMENDA SAMBAMBA NA KUMUENZI DKT RAURENCE MTAZAMA GAMA

 Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Bi.Maimuna Tarishi ,alisema  tamasha la makumbusho ya Taifa ya Majimaji yanakwenda sambamba na kumuenzi Dkt Raurence Mtazama Gama kwa mambo mengi ya maendeleo aliyoyafanya enzi ya uhai wake.Alisema Dkt Gama atakumbukwa kwa mambo mengi yakiwemo Uwanja wa michezo wa Ally Hasani Mwinyi Tabora,majimaji na zimani moto Songea..
 Aidha alisema masuala ya utalii yalikuwa mikoa ya kaskazini na Magharibi,lakini sasa Makumbusho ya kusini yatakuwa ni kivutio kikubwa cha utalii wa utamaduni.
Alisema tangu makumbusho ya majimaji yawe makumbusho ya taifa wageni wengi wandani na nje wametembelea katika makumbusho hayo. kutoka watalii 48 mwaka 2006/7 hadi 1,444.mwaka 2011.na kwamba Bodi ya makumbusho itaendele kutoa ushirikiano wa kutosha katika kuboresha vivutio vya kitalii katika kanda ya kusini.
 Wazee wa mila wa kingoni wameketi kwenye nyumba ambayo kumehifadhiwa vitu alivyokuwa akitumia Dkt Raurence Mtazama Gama.watalii wanafika kuona baadhi ya zana ambazo alitumia katika uhai wake,na ndiyo mwanzilishi wa makumbusho hayo.
 Kushoto ni mkuu wa wilaya ya Songea Bwana Ole Thomas Sabaya,wakatikati ni Chief wa Kingoni Emannuel Gama na Kulia na mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Thabit Mwambungu wakielekea  makumbusho ya majmaji mashuja Mahenge Katika Manispaa ya Songea.
Wanaingia katika maeneo ya mashujaa
 Katibu mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Bi Maimuna Tarishi akiwa katikati ya Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Mwambungu kushoto na Chief wa wangoni Emannuel Gama kulia wakiwa maeneo waliponyongwa wapigania uhuru wakati wa vita vya majimaji
 Wazee wa kingoni wakionyesha jinsi walivyo weza kupambana na wakoloni wa kijerumani kwa kutumia silaha zao za jadi katika viwanja vya mashujaa wa majimaji.

Wangoni hao na silaha zao za kijadi,ambazo hutumiwa kama ngoma ya Ligiu.yenye asili ya Afrika Kusini ambako walikimbia utawala wa Chaka Zulu.Hata hawa wanaimba nyimbo za kizulu.

No comments:

Post a Comment