Thursday, February 2, 2012

MAJAMBAZI SITA MBARONI KWA RUVUMA KUJERUHI NA KUPORA ZAIDI YA 4 MILIONI KWA TUMIA MILIPUKO


WATU sita ( 6 ) wanashikiliwa na Jeshi la Polisi wakituhumiwa ujambazi wa kutumia milipuko,mapanga na visu,Mkongotema Tarafa ya Madaba Mkoani Ruvuma usiku wa kuamkia tarehe moja Februari mwaka huu.
Kamannda wa Polisi wa mkoa huo,Kamanda Michael Kamuhanda amewambia wandishi wa habari kuwa majambazi hao kabla ya kufanya uhalifu huo walipofika kwa Bwana Remigius Ngunja walipiga milipoko mine hewani kutishia wanakijiji wasiweze kutoa msaada.
Kamanda Kamuhanda aliyataja majambazi yahu kuwa ni pamoja na Baraka Beda ( 25 ) mkazi wa Morogoro,Salum Ahmadi ( 45 ) mkazi wa Mtwara na Stanley Mtega ( 20 ) mkazi wa Ludewa.
Na wengine walikamatwa kwenye msko wa polisi ni pamoja na Peter Mbilinyi ( 25 ) ,mkazi wa Mkongotema,Mfalme Rashidi ( 30 ) mkazi wa Hanga Ngadinda na Jemsi  Mtewele ( 21 ) mkazi wa magingo.
Alisema wote kwa pamoja wako mahabusu wakati upelelezi ukiendelea,kwa tuhuma za kukutwa na  milipuko ,ambayo hutolewa kwa kibali kwa wachimba madini,barabara ,na vikosi vya usalama.
Alisema majambazi hayo yalikwenda nyumbani kwa Bwana Remigius Nguja na kuwamuru atoe fedha,aliposita basi walimkatakata kwa mapanga kichwani,mgongoni na mikononi,kisha wakamwendea mkewe Bibi Oktaviana Danda  wakamtishia kuwa watamkata mikono ndipo walipowapa zaidi ya shilingi 3,000,000 na kutokomea gizani.
Baada ya bkufanya uhalifu hu walikwenda kwa nyumbani kwa Bwana  Igno ambapo walimkuta mlinzi Bwana Awito Mbilinyi,kwa kuona hivyo aliwaonyesha kwa boss kwa kuwa hawamjui naye aliwaambia Boss hayupo labda mkamuulize mke wake.ataambia alipo.
 wakamuuliza boss wako yuko wapi,
Kamuhanda alisema majambazi hayo yalikuwa yakifuatilia fedha shilingi 15 milioni ambazo walisikia mtu mmoja katika kijiji hicho anazo bila ya kuwa na uhakika na mwenye fedha.
 Walipomwendea mke wa Igno kumuuliza Igno alipata mwanya wa kutoroka majambazi ,Mkewe alibakia na kizazaa cha kuonyesha fedha zilipo, na kuporwa shilingi 1,026,000.
Aidha Kamuhanda alisema baada ya msako wa polisi wa Madaba wakishirikiana na Polisi wa Songea Mjini , waliwakuta watuhumiwa kwenye gari lenye namba za usajili T.435DHT Costa ya kutoka Madaba kwenda Songea

No comments:

Post a Comment