Sunday, February 26, 2012

JUMAPILI YA KWANZA YA KWARESMA ,NI KIPINDI CHA MAJUTO ,KUJICHUNGUZA KATIKA DHAMIRA ZA WA KRISTO WA ROMAN CATHOLIC DUNIANI NAWATAKIA MFUNGO MWEMA

 Waumini wa Roman Catholic katika kanisa kuu la jmbo la Songea wakienda kupaka majivu Jumatano ya majivu ni ishara kuwa ni siku ya waumini hao kuanza mwezi wa toba na mfungo.Ambapo leo ni Jumapili ya kwanza ya Kwaresma Ibada iliyo adhimishwa kwenye makanisa ya RC Duniani kote.
 Askofu Mkuu wa Jimbo kuu la Songea Norbert Mtega aliwasihi waumini wake kuwa na toba ya kweli,na wala siyo kujionyesha kuwa unafunga,ni siri ya yule anaye funga na Mungu wake.Na kwamba amaomba amani hasa kipindi cha vurugu zilizotokea Katika manispaa ya Songea zilizosababishwa na maandamano ya kupinga mauaji.
Kila muumini wa dhehebu hilo hupakwa majivu kichwani kwa alama ya msalaba, ambao Yesu kristo alipigiliwa misumari mikono yake na miguuni.kama unavyo muona huyo muumini aliyekwisha pakwa majivu kichani.

No comments:

Post a Comment