Friday, February 17, 2012

SERIKALI IMEWATAKA WAKULIMA WA KOROSHO KUVUTA SUBIRA WAKATI IKITAFUTA UFUMBUZI WA KUPATA BEI ITAKAYO WANUFAISHA

Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Bwana Said Thabit Mwambungu

WAKULIMA wa Korosho Nchini wametakiwa kuwa na subira wakati huu mgumu
wakati serikali ikiendelea kutafuta suluhisho la kudunmu la kuwa na soko
la uhakika wa mazao hayo.

Wakati hayo yakiendelea tayari wakulima wa zao hilo wapo katika
mkanganyiko wa sintofahamu juu ya hatima ya soko la mazao yao ambayo
wengine wakiwa wanasubiri malipo ya awamu ya pili huku kukiwa na kundi
kubwa pia la wakulima waliopunjwa nguvu zao na vyama vikuu vya ushirika
kwa matumaini ya kuwalipa baada ya kuuza korosho hizo kwa wanunuzi
wakubwa.

Hayo yamesemwa na imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Bw. Said
Mwambunmgu wakati akiongea na Madiwanai wa Halmashauri ya Wilaya ya
Tunduru Mkoani humo na kuongeza kuwa hali hiliyo imetokana na Serikali
kubaini tatizo la ubabaishaji wa Soko la Mazao hayo katika msimu wa
Mwaka 2011/2012 hali inayo tishia wakulima kuapata malipo ya pili.

Sambamba  na ahadi hiyo pia Mkuu huyo wa Mkoa wa Ruvuma amewaahidi
wakulima wa mazo hayo kuwa kauli ya serikali juu ya Suluhisho la
kupatikana kwa Soko la uhakika litatolewa katika kikao kitakachoketi
February 2 Mwaka huu Mjini Dodoma  na kuwahushisha Wakuu wa Mikoa
Mitano inayao lima Korosho nchini.

Akifafanua taarifa hiyo Mkuu wa Mkoa huyo alisema kuwa kikao hicho
ambacho Mgeni Rasmi atakuwa Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Prof.
Jumanne Maghembe, Pia kitaweahusiha Maafisa Kilimo wa Mikoa na Wilaya
husika, wadau na viongozi wa vyama vya Ushirika katika Wilaya na Mikoa
hiyo.

Bw. Mwambungu aliitaja Mikoa itayaohusika katika Mkutano huo kuwa ni
Ruvuma, Mtwara, Lindi,Pwani na Morogoro  ambao alidai kuwa pamoja na
utekelezaji wa majukumu yao ya kawaida pia kwa pamoja wameapa
kutolifumbia macho suala la ubabaishaji wa soko la mazao hayo kutoka
kwa wakulima zikiwa ni juhudi za kuwarudishia ari wakulima baada ya
kuhakikishiwa upatikanaji wa soko la mazao yao ( source Steven  Augustino  Tunduru )


No comments:

Post a Comment