Wednesday, February 22, 2012

SIJAWAHI KUSHUHUDIA MABOMU YA MACHOZI YANAVYO WASHA MACHONI LAKINI LEO NIMESHUHUDIA,POLISI WALIPO KUWA WAKIRUSHA MABOMU HAYO LEO SONGEA MJINI

Hilo ni moja ya gari la polisi ambalo lilikuwa likigawa mabomu kwa wananchi walioandamani kupinga vifo vya watu vilivyotokea katika Manispaa ya Songea,Lizaboni juzi,Ruvuma jana na Mjimwema leo.
 Vijana hao wenye yeboyebo ndiyo waliyoanzisha  zali hilo baada ya mwendesha yebo mwenzao kuuliwa leo na kutupwa kwenye mto wa Matarawe.
 Wananchi waliyo fukuzwa kutoka stendi kuu ya mabasi wakiwa barabarani,lakini polisi kila walipokuta mkusanyiko waligawa mabomu hayo,inaelekea yalikuwa mengi na hayajatumika,na askari nao toka watoke kwenye mafunzo walikuwa hawajapata kashikashi kama ya leo.Ambapo katika vurugu hizo watu wawili wamepoteza maisha na wengine kadhaa wamepata majeraha mbalimbali sehemu zao za mwili.
 Hao ndiyo yebo yebo,hali tete katika Manispaa ya Songea imeonysha wananchi kuwa serikali ipo,na serikali nayo imetambua kuwa wananchi wakuchoka wanafanya matukio yasio na msingi kama hawatekelezewi kero zao.
Hili ni eneo maarufu sana katika Manispaa ya Songea kwa uuzaji wa mitumba,Majengo mabapo huwa watu wanajaa wateja na wauzaji wa nguo hizo,lakini leo hali ndiyo hiyo,kweupe kutokana na polisi.Shughuli zote za uzalishaji mali hazikufanyika kuanzia asubuhi hadi jioni.

Jamani amani bado inatakiwa Tanzania sijui wale wenzetu kila siku wanakimbia wanaisha vipi,sisi tulikuwa kwenye chumba cha mikutano lakini bomu la machozi lilitupwa nje bila sisi kujua,kilichotokea wote tulilia tukawahi kwenda kunawa maji.
Bunduki haina urafiki,ukimwona hata rafiki yako ameishika na kukulenga ujue uko katikati ,ya dunia na mbingu.Hadi hali inatulia mji mzima unanuka mabomu.

No comments:

Post a Comment