Sunday, February 26, 2012

MATUKIO WIKI ILIYO PITA KATIKA MANISPAA YA SONGEA KAMA HIVI ! !

 Askari polisi akionyesha karatasi yenye maandishi ya kiarabu ya tuhumiwa kwa waandishi wa habari katika Hospitali ya mkoa Songea  siku ya vurugu ya maandamano ya kupinga mauaji,baada ya kuwasachi watuhumiwa na kukutwa na hirizi ambayo kwa imani yao ilikuwa ikiwasaidia katika kifanya mauaji na maovu mengine bila kutiwa mbaroni lakini za mwizi ni arobaini.
 Gari la Polisi ambalo lilikuwa likitumika katika kutuliza maandamano siku hiyo ya machafuko katika manispaa ya songea Mkoani Ruvuma.kwa piga risasi hewani na kutupa mabomu ya machozi.
 Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Bwana Said Thabit Mwambungu akilikuwa akiongea na Kamati ya ulinzi na   usalama ya mkoa na wilaya na viongozi wa serikali wa mkoa na wilaya wakiwemo maafisa Tarafa,watendaji wa kata,Vijiji na mitaa siku ya vurugu hiyo kwa lengo la kurudisha amani iliyokuwepo hapo awali.
 Baada ya tukio hilo Mkuu wa Mkoa alitoa taarifa kwa vyombo vya habari na kutoa taarifa kwa wananchi wa Mkoa wa Ruvuma kuwa wawe watulivu,wasubiri serikali ifanye kazi yake ya kuwasaka wahalifu kwa kushirikiana na wananchi wenyewe pamoja na polisi.
Baadhi ya wananchi katika Stendi kuu ya Songea siku ya maandamano hayo wakati hali hajawa tete sana na mabomu yalikuwa bado kutupwa mfululizao,maana baada ya masaa manne yaliyo fuata hapakuwepo mtu alionekana katika maeneo hayo.
 Mkuu wa mkoa akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake siku hiyo isiyo sahaulika na wakazi wa Manispaa hiyo.
 Bwana Fili Karashani wa kwanza aliyesimama kulia,akiongea na waandishi wa habari wa Chama cha Waandishi wa Habari Ruvuma Press Club  katika ukumbi wa SACCOS ya walimu Majengo siku ya kwanza ya mafunzo ya habari za uchunguzi,na ndiyo ilikuwa siku ya vurugu hizo hivyo Bw.Karashani aliwaambia waandishi hao kwenda kwenye matukio na kisha warudi na habari za vurugu hizo ikiwa ni sehemu ya mafunzo kwa vitendo siku hiyo.
Kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa na wilaya siku ya machafuko hayo wakiwa katika ukumbi wa Songea Club na viongozi wengine wa mkoa na wilaya na watendaji wa vijiji,kata na mitaa kwa ajili ya kuleta amani.

No comments:

Post a Comment