Sunday, February 12, 2012

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI MKOANI RUVUMA KUHUSU ZIARA YA MAKAMU WA RAIS DKT MOHAMED GHARIB BILAL MKOANI RUVUMA

 Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mhe.Said Thabit Mwambungu akiongea na waandishi wanachama wa Ruvuma Press katika ukumbi wa maliasili kuhusu ziara ya Makamu wa Rais Dkt Mhe.Mohamed Gharib Bilal mkoani Ruvuma.
 Waandishi wa habari wakimsikiliza mkuu wa mkoa wa Ruvuma.
 Afisa Habari wa mkoa wa Ruvuma Bwana Kasimba
 Kaimu RAS wa Mkoa wa Ruvuma Dkt Anselim Tarimo akisisitiza jambo.
 Meza kuu wakisililiza hoja mbalimbali kutoka kwa waandishi wa habari hao
Mheshimiwa Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Thabit Mwambungu

MKUU wa mkoa wa Ruvuma Mheshimiwa Said Thabit Mwambungu amewatangazia wananchi wa mkoa wa Ruvuma kupitia vyombo vya habari mkoani Ruvuma kuwa kutakuwa na ziara ya kikazi ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt Mohamed Gharib Bilal siku ya Jumanne.
Mkuu wa mkoa huyo alisema  saa 5.00 asubuhi Makamu atapokelewa uwanja wa ndege na viongozi wa mkoa,kisha kuelekea Ikulu ndogo,kisha atatembelea hifadhi ya Taifa ya chakula Ruhuwiko na jioni wataweka jiwe la msingi ukumbi wa mikutano wa Manispaa, kusalimia wananchi kisha  kurudi Ikulu ndogo kwa mapumziko.
Alisema kuwa siku ya pili ya ziara hiyo Makamu ataondoka kwenda wilaya ya Namtumbo – Likuyu Sekamaganga hadi kwenye mradi wa URENIUM wa Mkuju na kusomewa taafa ya mradi na kukagua eneo la mradi huo ,kisha kurudi Songea.
Aidha siku ya Alhamisi Makamu ataelekea wilaya ya Mbinga ambapo atasomewa taarifa ya wilaya katika gereza la Kitai ,kukagua miradi kisha kuelekea Ruanda TANCOAL kupata taarifa ya makaa ya mawe,kisha kurudi Mbinga ambapo atazindua mashine za kuzalisha umeme.ambapo siku ya ijumaa atafanya majumuisho ya ziara yake katika ukumbi wa UMATI ,hatimaye atarudi uwanja wa ndege Songea na kuagwa na viongozi  na wananchi wa Mkoa wa Ruvuma.

No comments:

Post a Comment