Sunday, February 19, 2012

JKT MLALE YAINGIA FAINALI KATIKA 9 BORA BAADA YA KUMCHAPA POLISI YA IRINGA GOLI MOJA KWA SIFURI KATIKA UWANJA WA MAJIMAJI MJINI SONGEA

 Ni hicho kikosi kilicho pata tiketi ya kuingia 9 bora wakishika nafasi ya pili katika kundi lao ,anayeongoza ni Mbeya City.
 Wakitoka kwenye chumba cha mapumziko wakiingia uwanjani kumalizia kipindi cha pili.
 Furaha ilivyo wajaa wajeshi hao walipofika kambini kwao Uwanja wa Sabasaba - Matarawe  Katika Manispaa ya Songea.
Waliondika kwa mtindo huo ,ambapo kila mmoja alicheza alivyofikiri kwakuwa hakukuwa na ngoma.Ila kwa kawaida wajeshi hawahitaji ngoma,maana wanaweza wakacheza kwa mtindo wa kwata.Nakumbuka na mie nilipitia katika Jeshi hilo Ruvu JKT.




TIMU ya Jeshi la Kujenga Taifa ( JKT ) Mlale imeingia katika tisa bora katika kundi lao,baada ya kuifunga timu ya Polisi ya Iringa bao moja kwa sefori katika uwanja wa Majimaji Mjini Songea leo.

JKT Mlale ilipata goli la kwanza katika kipindi cha kwanza kwenye dakika 10 lililofungwa na mchezaji namba 3  Ahamad Kibopile,Polisi walijitahidi kurudisha goli lile lakini bahati haikuwa yao hadi mapumziko ikawa goli moja kwa bila..

Katika kipindi mchezo ukawa wakuvutia lakini JKT wakawa wakicheza mchezo wa kujihami zaidi,Lakini Polisi pamoja na ujanja wao haukuweza kufua dafu mbele ya vjiana wa JKT.Hivyo hadi firimbi ya mwisho goli ni moja kwa sufuri.Na kuwapa tiketi ya kuingia fainali,ambapo Mbeya City ndiyo wa kwanza wakiwa na point 22 wakati JKT wanapoint 16.

No comments:

Post a Comment