Sunday, February 19, 2012

BREAKING NEWS !!! WANAUME HUKO KENYA ( NYERI ) WANAPATA KIPIGO CHA KUFA MTU TOKA KWA WAKE ZAO WANAPOTOKA KWENYE POMBE

 Tunaposema unyanyasaji wa kijinisia kwa wanawake na watoto kutoka kwa baadhi ya wanaume wenye mfumo dume,kwa upande wangu naona wanaume wanaonewa.Mfano mzuri ni kwa huyo mwanaume mwenzetu mwenyeji wa Nyeri jina lake halikutambulika alivyo fanana.je ndivyo alivyo zaliwa na mama yake hivyo.Basi kazi hiyo ni ya mkewe aliyoifanya kwenye uso na kichwa cha mmewe.kisa ati amerudi usiku,amelewa pombe.kisa hicho si cha huyo mwanaume mwenzetu tu yaliyomkuta wiki iliyopita bali waki wengi wanaume wamefanyiwa unyama huo na wakezo huku Nyeri Nchini Kenya.
Huyo naye ni mwnume aliyepata kisago kutoka kwa mkewe baada ya kurudi nyumbani kalewa pombe,yeye ambaye jina lake wanalo wenyewe Nyeri huko nchini Kenya .alipata dhahama hilo kisogoni,shingoni na kichwani ambapo kichwani alikula nyundo ya kichwa.

Wanawake hao wanasema wanaume wakileta za kuleta wanatandikwa.'Kama analeta fujo anapotoka kwenye pombe zake,nikiwa na chochote nitampiga nacho.Maana wao wanakunywa pombe,sisi ndiyo tunahangaika na watoto,kuchuma kahawa wao wanadai fedha za kunywea bila ya ustaarabu'.alisema mama mmoja ambaye hakufahamika jina lake.

Wasomaji wa Blog hii,ninani alaumiwe,mke au mme?,lakini kama ndivyo je adhabu hizo walizoziamua kuzitoa kwa wanaume wao huko Nyeri inafanana na kuadhibiwa,au ni uuaji? ( Source K24 )

No comments:

Post a Comment