Saturday, January 22, 2011

WANANCHI WA TUNDURU WAHAIDIWA HUDUMA YA BENKI YA CRDB

 Afisa wa Benki ya CRDB Tawi la Songea Bwana Gerald  Michael akitoa mada kwenye semina ya siku moja ya wadau wa Ushirika katika ukumbi wa Songea club
 Wajumbe wakisikiliza mada kuhusu huduma za benki ya CRDB
 Wajumbe wa semina ya siku moja ya wadau wa Ushirika wakijitambulisha kwa kikundi kwa mgeni rami
 Wajumbe wakijitambulisha kwa vikundi kwa mgeni rasmi katika ukumbi wa Songea club katika Manispaa ya Songea Leo
Mgeni Rasmi kaimu RAS wa mkoa wa Ruvuma Dkt Anselim Tarimo akisistiza umuhimu wa wananchi kupata elimu ya ushirika wa kuweka na kukopa,ili waweze kununu pembejeo za kilimo.ambapo Tunduru wanazao la korosho.Namtumbo tumbaku na Mbinga kahawa.

Naye 
Afisa wa Benki ya CRDB Tawi la Songea aliyemwakilisha Meneja wa Benki hiyo kwenye semina ya siku moja ya wadau wa ushirika mkoani Ruvuma leo Bwana Gerald Michael aliwaambia wanasemina wapatao 80 waliohudhuria semina hiyo kuwa Tayayari Jengo la huduma za kibenki linafanyiwa ukarabati wilayani humo. Alipojibu swali la mjumbe mmoja wa Tunduru.

Bwana Michael alisema huduma zao ni za uhakika na za usalama wa hali ya juu,isitoshe wanatoa mikopo kwenye SACCOS na wafanya kazi ambao waajiri wao wameingia mkataba nao.

Alisema hayo wakati akitoa mada yake kuhusu huduma zinazotolewa na Benki ya CRDB kwa washiriki kutoka vyama vya ushirika,SACCOS,VIKOBA,na taasisi nyingine za kifedha na vyama vya ushirika vya kuweka na kukopa.

No comments:

Post a Comment