Monday, January 31, 2011

BREAKING NEWS,PROFESA ANNA TIBAIJUKA AJA NA MPYWA KWA WAKAIDI WA KUNG'OA MAWE BIKONI

  1. a
  2. Mheshimiwa Profesa Anna Tibaijuka waziri wa Ardhi nyuma na makazi ,anasema kama askari wa usalama barabarani  Traffic wanaangalia uasalama barabarani kwanini basi kada ya askari wa Ardhi na makazi wasirejeshwe kazini. 
  3.  
    Askari wa ardhi na makazi warejeshwa kazini,ili kuangalia ukiukwaji wa sheria za ujenzi uliwekwa kisheria na serikali.

    Waziri wa Ardhi na makazi Mhe.Profesa Anna Tibaijuka alisema katika mahojiano na ITV kuwa kada hiyo ilisahaulika hapo awali lakini sasa watarudi kazini kwakuwa kuna watu wenye kiburi cha kung’oa mawe yanayowekwa kwa tamaa yakupanua kiwanja chake.

    Alisema kama mtu yupo tayari kuishi mjini basi afuate kanuni na sheria za ardhi za kuheshimu mipaka ya viwanja vyao.Hatupo hapa kwa kukomana bali tunafanya  kazi kwa kushirikiana na wananchi.

    Aidha alisema kutaundwa Programu ya kuwawezesha vijana nyumba au kiwanja,katoa mfano kupata nyumba Kinondoni ama kiwanja Bunju.

    Profesa Tibaijuka alisema anafanya kazi aliyopewa na Rais.na hafanyi kazi njia za mkato ( short cut ),short cut zimeshapitwa na wakati kitakacho takiwa ni kufuata sheria za ardhi na nyumba na makazi.pia lasema kazi katika sekta hiyo si ya kukomoana,bali ni kutoa elimu kwa wananchi ya kujua haki zao

No comments:

Post a Comment