Monday, January 10, 2011

WAHADHIRI NA WANACHUO UDOM WAGOMA KUDAI POSHO NA MASLAHI

Hivyo migomo ndiyo njia pekee ya usuluhisho wa kupata haki za watu?,katika taasisi za serikali au taasisi binafsi?,Ifike mahali sasa Serikali na vyombo vyake kukaa chini na kutafuta vyanzo vya migomo,na kulitafutia suluhisho.Mgomo wa UDOM ni wa pili ukifuatiwa na huu wa sasa.wanafunzi wa Kitovu cha Social waligoma kudai fedha za Field nasikaia Serikali ikawalipa.

Kwa mtindo huo,hata Wahadhiri nao wameamua  kuungana na  wanachuo ambao wanamadai mbalimbali ili walipwe  stahili  zao au madai yao. Kama ndivyo kwanini  Serikali na vyombo vyake vingojee migomo ndipo malipo yafanyike? Sijui  wewe na mimi  tunalionaje jambo hili?.litaendelea hadi lini? Ni nani alaumiwe wahadhiri,wanachuo ama Serikali?

No comments:

Post a Comment