Monday, January 31, 2011

Dhana ya kuchimba dawa kwa wasafiri wa mabasi hakuhitaji Hotel au toilet

Hao ni wasafiri kutoka Songea kwenda Dar esa salaam,kama kilometa chache kufika Njombe Dereva wa Basi la Summry  alisimamisha busi na abiria wakaenda kujisaidia,na mara nyingi ni haja ndogo maarufu kwa jina la kuchima dawa. kuna kosa gani?
 
Sasa Dhana hiyo inazua mijadala kibao miongoni mwa watu,na wengine hawaja wahi kusafiri umbali mrefu kuanzia saa 12 asubuhi hadi saa 2 usiku ama siku mbili njani.Ikumbukwe basi linabeba abiria wakila sampuli,kuna wazee,watoto,wagonjwa ndiyo maana kuchimba dawa kutabakia kama kulivyo,kutokana na mazingira ya usafiri yalivyo.
 
Maoni ya wadau wengi wanadai wajenge maeneo maalumu ya kuchimba dawa hilo sipingi,daharula ikitokea kwa abira kushikwa tumbo la kuharisha na kituo cha kuchimba dawa kilicho andaliwa kiko mbali je huyo abiria atakuwa katika hali gani?

No comments:

Post a Comment