Sunday, January 30, 2011

BINADAMU TUWE NA HURUMA KAMA ANAVYO TUHURUMIA MUNGU

Binadanu hatuhurumiani wenyewe kwa wenyewe,ni marangapi binadamu anaanguku kwa dhambi,anamkosea Mungu lakini Mungu anatoa msamaha,hayo ni baadhi ya mahubiri ya Padre ( Rv.Degratias Nditi ) Padre anayefundisha Seminari Kuu ya Peramiho katika Kigango cha Matarawe katika Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma leo.

Baba Padre Nditi  alirejea  MISALE YA WAUMINI Somo la leo '  Heri wenye Heri:' maana  hao watapata Rehema':ina maana wale ambao wanahuruma na wao watahurumiwa siku yaka.Ailsema huruma isipokuwepo na visasi vitatawala.' ni marangapi ukienda vijijini wananchi wanalalamika mazao yao yanakosa mbolea.wakati viongozi wasio na huruma wanagawa mboleakwa njia zisizo eleweka na kufurahia?' alisema.

Alisema nchi kama Tunisia wananchi wako katika machaufuko ya Kisiasa ni kwa sababu viongozi wao hawana huruma kwa wananchi wao,hali kama hiyo haiendi na mifano ya Mungu anayetuhurumia wakati sisi tuna mkosea,tunamchukiza kwa maovu tunayo mtendea kila mara.

No comments:

Post a Comment