Tuesday, January 25, 2011

HII NDIYO MAKUMBUSHO TA TAIFA YA MAJIMAJI SONGEA ( SONGEA NATIONAL MESEUM)

 Ndani ya jengo hilo kuna masalia na zana mbalimbali wangoni walikuwa wakitumia ni pamoja makabila yote ya mkoa wa Ruvuma vya utamaduni wao,
 Hiyo ni nyumba ya kimila ya wangoni ambayo wangoni walikuwa wakijenga katika  Kingdom  zao waliosimama ni wa zee wa kimila wa kingoni mwenye kaunda suti ni mzee John Joseph Gama Makamu mwenye kiti wa Makumbusho ya Majimaji. wapili mwenye kamtule ni mzee  Crispin creophas Mahuna.
 Hilo hapo ni kaburi la cheif wa kingoni Songea  Luwafu Mbano ambaye alizikwa pekeyake katika kaburi hilo.
  hilo ni kaburi lililo zikwa machifu,nduna 66 katka kaburi moja ( kaburi la halaiki) Mass grave.
 Hiyo ni sanamu inayo wakilisha askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania waliokufa katika vita vya Idd Amin wa Uganda
Hapo ni ofisini kwa mkurugenzi wa makumbusho hayo Bwana Philip maligisu aliye vaa nguo nyeusi nakaimu mwenyekiti Mzee Joseph Gama mwenye kofia aliyeshika kitabu akimkabidhi Mwenye kiti wa Press Club Ruvuma Bwana Juma Nyumayo hayupo taika picha.



Makumbusho ya Taifa ya Majimaji yana madhumuni ya kutunza,kuhifadhi ulithi na utamaduni wa mtanzania.

Madhumuni mengine ni Taasisi ya makumbusho ya taifa kama mhifadhi namba moja wa urithi wa mtanazia.

Mkurugenzi wa Makumbusho ya majimaji Bwana Philip Maligisu anasema kazi zilizopo katika makumbusho hayo ni pamoja na kukusanya rasilimali za utamaduni wa mtanzaia.

Pia pamoja na kutoa elimu kwa umma kuhusu urithi wa utamaduni wa asili,kufanya utafiti na kuhifadhi kumbukumbu muhimu ili ziwe salama kwa niaba ya Umma.

Kushirikisha watanzania kupitia Program za utamaduni ili kuonyesha jamii utamaduni wa mtanzania,ili kufungua mtandao mpana wa ndani na nje ya nchi ( Network system ).

Pia wananchi waweze kuelewa na kuanzisha makumbusho ya Taifa katika wilaya ambapo tarehe 22 hadi 23 wadau wa makumbusho watakwenda wilaya ya Mbinga kuanzisha makumbusho ya Taifa katika wilaya hiyo mkoani Ruruma kwakuwa wao wamesha fikia katka sifa ya kuanza makumbusho yao.

Kwa kuwa wilaya hiyo itakuwa karibu na wilaya mpya ya Nyasa wataweza kupanua utalii kupitia ziwa nyasa,makaa ya mawe na uoto wa asili ambao utawavutia watalii..

Bwana Philip alisema makumbusho haya yalianza kabla ya ukoloni kwa sheria namba 40 ya mwaka 1936,na baadaye kutungwa sheria  Tanganyka namba 23 ya mwaka 1963  baada ya Uhuru.

Na baadaye sheria namba 37 ya mwaka 1965  ambayo ilikuwa na waziri mwenye Dhamana na makumbusho ya taifa na hatimaye seria namba 7 ya mwaka 1980 yakuwa na makumbusho ta Taifa ambayo yapo Dar es salam.

Makumbusho ya taifa ya  majimaji yatafungua wigo wa watalii kutembele Songe kuona wanya katika hifadhi ya Seluu,Ruhira ambako kuna hifadhi ya wanyama kama vile viboko na ndege wenye rangi za kuvutia.

No comments:

Post a Comment